• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wanaoharibu Vyanzo vya maji kukiona

Posted on: April 5th, 2018

Serikali mkoani Shinyanga imewaonya wananchi wote wakaohusika na uharibifu wa vyanzo vya maji kwa kufanya shughuli za kilimo na kunywesha mifugo kwenye vyanzo vya maji na kusababisha ongezeko la uharibifu wa mazingira.

Mhe. Zainab Telack ameyasema hayo mapema wiki hii, katika kijiji cha Songwa Wilaya ya Kishapu ikiwa ni maadhimisho ya upandaji miti kitaifa yaliyofanyika Wilayani humo.

Ameonya kuwa shughuli hizo zinahatarisha uhai wa vyanzo hivyo vya maji pamoja na uhai wa binadamu kutokana na matumizi ya madawa yanayotumika katika kilimo hicho.

“Kishapu mna mabwawa matatu lakini kwa bahati mbaya wachimbaji almasi na wanaolima kando kando ya mabwawa wameyaharibu, hivyo niwaombe kwa sababu tumetambua kuchimba kwenye mabwawa ni makosa na kulima ni makosa pia ni marufuku kufanya shughuli hizo,” amesisitiza.

“Mnapofanya kilimo cha nyanya au mahindi mnatumia madawa yenye sumu na kuyachafua maji kwa hiyo hayafai kutumika na siku hamna maji mnayatumia wakati huo mmeshaweka sumu, mnaogesha watoto wanapata madhara, acheni kulima kando ya mabwawa haya,” ameongeza Mhe. Telack.

Aidha, Mhe. Telack amesisitiza umuhimu wa kupanda miti kando ya vyanzo vya maji hasa mabwawa na kuwa ndiyo chanzo cha maji kwani husaidia yasikauke hivyo huwezesha mvua kunyesha.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mhe Nyabaganga Taraba amesema hapo nyuma wananchi hawakuwa na mwamko katika shughuli za uhifadhi mazingira hivyo kuchangia kuwa na mabadiliko ya tabianchi.

Mhe. Taraba amesema kuwa baada ya kupanda miti katika maeneo yanayozunguka bwawa hilo hatua hiyo imeweza kusaidia kurudi upya kwake na hivyo wananchi kuendelea kupata faida.

Amesisitiza kuwa suala la upandaji miti pamoja na utunzaji misitu ni la wananchi wote na ndio maana viongozi wote wanashiriki katika zoezi na kuahidi viongozi watandelea kuwa bega kwa bega kuhakikisha mazingira yanahifadhiwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUOMBA NAFASI YA UJUMBE WA BODI YA HOSPITALI YA MKOA January 03, 2020
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha nne 2019 January 09, 2020
  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa Kidato cha pili 2019 January 09, 2020
  • Mwenge wa Uhuru kuwasili Mkoani Shinyanga May 07, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU 100

    June 27, 2021
  • SIKU MIA 100 ZA RAIS SAMIA

    June 27, 2021
  • DKT. SENGATI AHAIDI KUPAMBANA NA CHANGAMOTO YA UMASIKINI SHINYANGA

    June 05, 2021
  • Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga aapishwa

    June 02, 2021
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa