• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WANASHINYANGA JITOKEZENI KWENYE UANDIKISHAJI WA WAPIGA KURA- RC MACHA

Posted on: September 5th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewaomba Wanashinyanga kwa ujumla wao kujitokeza na kushiriki kikamilifu kwenye zoezi la Uandikishaji wa Wapiga kuanzia tarehe 11 - 20 Oktoba, 2024 ili kuweza kuchagua viongozi mbalimbali katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba mwaka huu.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 5 Septemba, 2024 alipokuwa akihutubia wajumbe wa Kikao cha Wadau kilichokuwa kinajadili Mpango wa Matumizi ya Ardhi katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ambapo pamoja na ombi hili kwa wananchi lakini pia amewakumbusha kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali zitakazotangazwa.

"Niwaombe sana Wanashinyanga, tujitokeze kwa umoja wetu na kila mwenye sifa ya kujiandikisha kupiga kura aende katika maeneo yetu tunayoishi kuanzia tarehe 11 hadi 20 Oktoba, 2024 ili itakapofika wakati wa kuchagua viongozi aweze kutumia vema haki yake hiyo ya msingi," amesema RC Macha.

Aidha, RC Macha amesema kuwa baada ya kujiandikisha pia mwananchi anayo haki ya kugombea nafasi hizo za uongozi kupitia vyama vya siasa na baadae kutafuatiwa na zoezi la Upigaji wa Kura kuwachagua viongozi wa Serikali za Mitaa ifikapo tarehe 27 Novemba, 2024.

Kando na haya, RC Macha amewaomba wajumbe wote waliohudhuria kikao hiki kwenda kusaidia kutoa elimu kwa wananchi, wasaidizi wao na wale wote wanaowazunguka katika maeneo yao ili waweze kushiriki vema katika zoezi hili linalokuja huku akisisitiza kuwa Serikali nayo itaendelea na utoaji wa matangazo ya kuwakumbusha kushiriki kikamilifu wakati ukifika.

Ikumbukwe kwamba, mwaka huu ni wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao utafanyika tarehe 27 Novemba, 2024 nchini kote ambapo viongozi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji watachaguliwa kuongoza kwa kipindi cha miaka mitano ijayo ambapo Mkoa wa Shinyanga una jumla ya Mitaa 90, Vijiji 506 na Vitongoji 2749.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa