• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WATAALAM WETU, BADILIKENI - RC MACHA

Posted on: May 17th, 2024

Na. Paul Kasembo, Shinyanga DC.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka watalaam Mkoani Shinyanga kubadilika katika utendaji kazi wao na kutimizamwajibu wao kila mmoja kulingana na taaluma yake katika eneo lake badala ya kusubiria kuanza kusimamiwa, huku akimpongeza Lucia Mahena ambaye ni Mganga wa Kituo cha Afya Salawe kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa utendaji kazi mzuri anaoendelea nao.

Akiwa Salawe RC Macha amepata nafasi ya kuzungumza na wagonjwa ambao walikuwa hapa ambapo alitaka kujuwa kama wanahudumiwa vizuri, lugha zinazotumika wakati wakisubiri na wakati wakipata huduma kutoka kwa watoa huduma na kama wanapata dawa kadiri ya mahiaji yao ambapo wote kwa nyakati tofauti wamesema wanaridhishwa sana na ndiyo msingi wa RC Macha kumpongeza Daktari Lucia.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 17 Mei, 2024 wakati akikagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambapo ameanza na Kituo cha Afya Salawe kilichopatiwa zaidi ya Tzs. Bil. 1 kwa ajili upanuzi wa jengo la Wagonjwa wa nje, Maabara, Mochwari, Kichomea taka, Mama na mtoto, jengo la upasuaji pamoja na wodi ambapo mpaka sasa majengo yote yapo hatua ya umaliziaji.

Pamoja na maelekezo mengine, RC Macha ameishauri Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kuweka vipaumbele katika ujenzi wake huku akipendekeza kuanza na  jengo la wagonjwa wa nje pamoja na maabara ili kukabiliana na changamoto zilizopo hivi sasa katika Kituo hiki.

"Niwatake wataalam wote mbadilike katika utendaji kazi wenu wa kila siku, acheni kufanya kazi kwa mazoe, kuweni wabunifu, msiwe  timizeni wajibu wenu, toeni ushauri wa kitaalam hasa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na mshirikiane," amsesema RC Macha.

Aidha amemuelekeza Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jukius Mtatiro (Wakili) kukutana na wataaalm wote, mafundi na kamati zilizohusika ili kuona namna ya kuedelea na umaliziaji wa upanuzi wa Kituo hiki cha Salawe ambacho inatajwa kuwa kukamilika kwake kunakuja kuondoa adha ya upatikanaji wa baadhi ya huduma muhimu ambazo nyingine wanalazimika kuzifuata kwa zaidi ya KM 100.


HABARI PICHA



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa