• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI NA WALEZI WEKEZENI ZAIDI KATIKA MALEZI NA MAKUZI YA WATOTO – LYAMONGI

Posted on: May 15th, 2025

Na. Paul Kasembo, RS Shinyanga.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu, Ndugu David Lyamongi, aliyemwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga CP Salum Hamduni, amewataka wazazi na walezi kuwekeza kwa dhati katika malezi na makuzi ya watoto kuanzia wakiwa tumboni, ili kuimarisha maadili na kuleta tija kwa Taifa katika siku zijazo.

Lyamongi alitoa wito huo Mei 15, 2025 wakati akifungua Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Familia kwa Mkoa wa Shinyanga. Hafla hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Kalinjuna uliopo katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali wakiongozwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yudas Ndungile.

Viongozi wengine ni kutoka madhehebu ya dini, Kamati ya Amani Mkoa, wawakilishi wa Baraza la Wazee, Baraza la Watoto, Vyama vya Watu Wenyeulemavu, wadau wa maendeleo - Shirika la ICS, na Klabu ya Wandishi wa Habari, wataalamu wa masuala ya kijamii, wanafunzi kutoka vyuo na shule za sekondari pia walishiriki katika kongamano hilo ambalo lililenga kuhamasisha jamii kuishi kwa kuakisi kaulimbiu ya mwaka 2025: “Mtoto na Malezi: Msingi wa Familia Bora, Taifa Imara.”

“Niwatake wazazi na walezi wote mkoani Shinyanga kuhakikisha wanawekeza ipasavyo katika malezi na makuzi ya watoto wetu kuanzia wakiwa tumboni, ili tuweze kujenga Taifa lenye msingi imara wa maadili na maendeleo endelevu,” alisema Lyamongi.

Awali, akimkaribisha mgeni rasmi, Dkt. Yudas alieleza kuwa maadhimisho hayo yana lengo la kuwaleta pamoja wadau wote wa malezi ya watoto, kwa ajili ya kutafakari na kubadilishana uzoefu juu ya jitihada zinazofanywa katika kuimarisha malezi na makuzi bora kwa watoto.

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoa wa Shinyanga, Bi. Lydia Kwesigabo, alibainisha kuwa kila mwaka Mei 15, Tanzania huungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Familia, ikiwa ni fursa ya kutathmini mchango wa jamii katika maendeleo ya watoto na familia kwa ujumla.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

    May 20, 2025
  • SERIKALI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU SITA NA MAJERUHI 11 KATIKA AJALI YA MGODI WA MWAKITOLYO.

    May 18, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI, NENDENI MKAWE MABALOZI SAHIHI WA KAZI ZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – RC. MACHA

    May 16, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI WEKEZENI ZAIDI KATIKA MALEZI NA MAKUZI YA WATOTO – LYAMONGI

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa