• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAZIRI MHE. DKT. JAFO AWAKARIBISHA WATANZANIA KUTEMBELEA MAONESHO YA 49 YA SABASABA 2025

Posted on: July 2nd, 2025

#Sabasaba - 2025.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selamani Jafo, amewaomba na kuwakaribisha Watanzania wote kutoka mikoa mbalimbali kufika Jijini Dar es Salaam kushiriki Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea katika viwanja vya Mwl. Julius Nyerere, barabara ya Kilwa.

Akizungumza Julai 2, 2025 wakati wa ziara yake katika maonesho hayo, Mhe. Dkt. Jafo alisema Maonesho ya Sabasaba 2025 ni fursa muhimu kwa wananchi kutembelea, kujifunza, kununua bidhaa, kupata huduma mbalimbali za kijamii, pamoja na kujionea ubunifu wa bidhaa na huduma kutoka kwa washiriki wa ndani na nje ya nchi.

"Ni wakati muafaka sasa kwa Watanzania kutoka maeneo mbalimbali ya nchi kuja kujionea fursa zinazopatikana kupitia Maonesho haya. Kuna bidhaa, huduma, na maarifa mengi ya kujifunza pamoja na kujenga mitandao ya kibiashara," alisema Mhe. Jafo.

Aidha, amesisitiza kuwa Maonesho ya mwaka huu yanatoa taswira halisi ya maendeleo ya viwanda, biashara ndogo na za kati nchini, pamoja na jitihada za Serikali katika kukuza uchumi wa viwanda kupitia ushiriki wa wadau mbalimbali wa sekta binafsi na umma.

Maonesho ya Sabasaba ni jukwaa muhimu la biashara na uwekezaji, yanayowakutanisha wadau kutoka ndani na nje ya nchi, na hufanyika kila mwaka kwa lengo la kukuza ushirikiano wa kiuchumi na kukuza bidhaa za Kitanzania katika soko la kimataifa ambapo Mkoa wa Shinyanga unashiriki kikamilifu ukiwa na Mabanda 8.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM APONGEZA USHIRIKI WA MKOA WA SHINYANGA KATIKA MAONESHO YA SABASABA.

    July 06, 2025
  • RC. MBONI ATOA WITO KWA TISEZA KUTANGAZA FURSA KUU YA KONGANI YA UWEKEZAJI BUZWAGI

    July 05, 2025
  • MHE. RIDHIWANI KIKWETE AWAKARIBISHA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LA MKOA WA SHINYANGA KWENYE MAONESHO YA SABASABA

    July 05, 2025
  • KATIBU TAWALA WILAYA YA KAHAMA AWAPONGEZA WASHIRIKI WA MAONESHO YA SABASABA 2025 KUTOKA MKOA WA SHINYANGA

    July 05, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa