• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

ZAIDI YA SH. BIL. 5.9 ZIMETENGWA KWA AJILI YA MIRADI YA MAJI MKOANI SHINYANGA

Posted on: March 21st, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amesema Mkoa wa Shinyanga mwaka huu 2016/ 2017 umetenga shilingi 5,987,366,000 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Maji Mkoani hapa.

Mhe. Telack amesema hayo katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Josephine Matiro wakati uzinduzi wa wiki ya maji uliyofanyika Kimkoa katika Wilaya ya Shinyanga kwenye kata ya Usanda, kijiji cha Manyada.

Mhe. Telack amesema hadi sasa fedha iliyopatikana na inaendelea kufanyiwa kazi ni sh. 1,756,894,718 sawa na asilimia 29.3 ya bajeti..

Telack amewataka wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kuithamini miradi hii na kuitunza ili iwe endelevu kwani inatumia fedha nyingi.

“Viongozi wasimamie utekelezaji wa Sheria ya utunzaji wa mazingira ili kunusuru vyanzo vya maji kwani Serikali inatumia fedha nyingi katika utekelezaji wa miradi ya maji” Telack amesema katika hotuba yake.

Katika uzinduzi huo wa wiki ya maji Mhe. Josephine Matiro kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Zainab Telack, amezindua mradi wa maji ya bomba wa kijiji cha Manyada uliogharimu shilingi 629.8 milioni, ambao utawanufaisha wananchi 3,650 wa vitongoji saba wa kijiji hicho.

Aidha, Mhe. Matiro pamoja na msafara ulioambatana naye, wamepanda miti katika chanzo cha maji cha mradi huo ili kwa lengo kutunza mazingira ya chanzo hicho.

Akizungumzia hali ya maji kwa sasa Mkoani Shinyanga, Mtaalamu wa maji katika Sekretarieti ya Mkoa, Bw. Marwa Kisibo amesema kuwa, kwa sasa hali ya upatikanaji wa maji mijini ni asilimia 68 na vijijini ni asilimia 52.

Ameongeza kuwa, Serikali ina mpango wa kufikia asilimia 85 ya upatikanaji wa maji vijijijini na asilimia 95 mijini kufikia mwaka 2020 kutokana na program ya maji inayojulikana kama WSDP (Water Sector Development Program) iliyoanza mwezi Julai, mwaka jana 2016.

Amesema kuwa, program hiyo imelenga katika kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji mijiji na vijijini.

Naye Katibu wa Kamati ya maji ya Kijiji cha Manyada Bw. John Daniel amesema mradi huu utawanufaisha sana wananchi wa kijiji hicho na kuiomba Serikali kuwasaidia kupata umeme kwa ajili ya kuendeshea mtambo wa kusukuma maji badala ya kutumia mafuta ya Dizeli.

Kauli mbiu ya wiki ya maji mwaka huu ni “Maji safi na maji taka, punguza uchafuzi yatumike kwa ufanisi”.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa