• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Zaidi ya sh. mil. 20 zachangwa ujenzi wa jengo la wanafunzi wenye mahitaji maalum

Posted on: October 14th, 2017

Jumla ya sh. Milioni 20.6 kati ya hizo, fedha taslimu zikiwa mil. 10.8 na ahadi sh. Mil. 9.4 na mifuko 465 ya saruji yenye thamani ya sh. Milioni 6.8 zimechangwa katika harambee maalumu iliyofanyika wakati wa mahafali ya kidato cha nne na maadhimisho ya miaka 50 ya shule ya Sekondari ya Shinyanga iliyopo katika Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga.

Harambee hiyo imefanyika jana tarehe 13/10/2017 na kuongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack kwa lengo la kukusanya fedha kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa nyumba mbili za kuishi walimu kila moja yenye uwezo wa kubeba familia 5, ujenzi wa jengo la maabara ya Zahanati na vyumba vitatu vya kupumzisha wagonjwa pamoja na jengo la wanafunzi wenye mahitaji maalumu.

Kabla ya kuendesha harambee hiyo, Mhe. Telack amesema kuwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu ni sawa na watoto wengine kiakili hivyo wanahitaji miundombinu itakayowawezesha kutekeleza vema majukumu yao wakiwa shuleni.

Aidha, amewataka wahitimu kutumia mitandao ya kijamii kutafuta fursa za maendeleo na masomo ya juu badala ya kutumia kwa mambo yasiyo ya faida kwao.

Mgeni rasmi wa shughuli hiyo Dkt. Charles Kimei aliyewakilishwa na Bw. Phillip Magani kutoka benki ya CRDB makao makuu katika hotuba yake amesema ni fahari na furaha kwa nchi yetu kwa shule ya Shinyanga Sekondari kufikisha miaka 50 kwani imeweza kusomesha maelfu ya Watanzania ambao wengi wao ni viongozi na watendaji wakubwa katika Sekta mbalimbali nchini na hata nje ya nchi.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Taraba amewataka wanafunzi wa miaka ya nyuma wa shule hiyo akiwemo Dkt. Kimei kutosahau walipotoka na kuwasisitizwa kuwa shule ya “ShyBush” inawahitaji kusaidia katika juhudi za maendeleo kwani ni shule ya Watanzania wote.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa