• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

AEK NA WAKUU WA SHULE, BANDIKENI ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ILI TUJUE NANI HAJAJIUNGA NA KWA NINI -RC MACHA

Posted on: March 3rd, 2025

Na. Paul Kasembo, MSALALA DC

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule za Sekondari mkoani Shinyanga kubandika orodha ya majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na shule ili kuwabaini wale ambao bado hawajiunga na hatua za kisheria zichukuliwe kwa wazazi ambao hawajawapeleka watoto wao shule.

RC Macha ametoa wito huo Machi 3, 2025 wakati akiweka Jiwe la Msingi katika Shule ya Sekondari Bumva iliyopo Kata ya Segese Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambapo ameendelea kutoa wito kwa wazazi kuwapeleka shule watoto wa kike na wa kiume badala ya kuwapeleka wakachunge ng’ombe.

“Ninawaagiza Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule za Sekondari wote mkoani Shinyanga kubandika orodha ya wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na shule ili tuwabaini wanafunzi ambao bado hawajajiunga na shule ili hatua za kisheria zichukuliwe kwa wazazi ambao hawajawapeleka watoto shule”, amesema RC Macha

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Hamduni amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kufanya kazi kubwa ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Elimu kwani alitoa takribani Bilioni 6 kwa ajiri ya ujenzi wa Shule 8 za Kata ili kuwawezesha wanafunzi kunufaika na elimu bora.

Akiwasilisha taarifa ya ujenzi, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mwl. Nyerere Kafuru Songora amesema ujenzi huu ulianza kutekelezwa Novemba 19, 2024 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Machi 10, 2025 ambapo wanafunzi wa Shule ya Mwalimu Nyerere, Segese na wanaokaa maeneo ya karibu wataanza kusoma mara moja kwani tayari shule hii imeshasajiliwa kwa namba ya usajili S. 6824.

Mradi huu wa ujenzi unatekelezwa kwa kutumia Mfumo wa Force Account ambapo mpaka sasa ujenzi umegharimu takribani Milioni 603 ukihusisha ujenzi wa Jengo la Utawala,Vyumba vya Madarasa, Jengo la Tehama na Maktaba, Vyoo na kichomea taka, Tanki la maji pamoja na Jengo la Maabara.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa