• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

EACOP NA AMEND SHIRIKISHENI WANANCHI MNAPOTEKELEZA MRADI – RC MACHA,

Posted on: November 15th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka wasimamizi wa Shirika lisilokuwa la Kiserikali linalotoa Elimu ya Usalama Barabarani kwa Jamii (AMEND) - Mkuza wa Bomba la Mafuta ghafi Afrika Mashariki (EACOP) kuhakikisha kuwa wanashirikisha wananchi wanapotekeleza mradi huu hapa mkoani Shinyanga ili kulinda usalama wao na mali zao katika maeneo ambapo mradi huu unatekelezwa.

Ameyasema haya leo tarehe 15 Novemba, 2024 kwenye kikao cha wadau wa Mkoa wa Shinyanga kikao ambacho kimelenga kuwashirikisha na kupokea mapendekezo kuhusu namna ya kuboresha usalama katika jamii ili kufanya Mkoa ubaki salama kwa muda wote ambao mradi wa EACOP utakuwa unatekelezwa.

“Niwaombe ninyi wasimamizi wa mradi wa EACOP na Shirika la AMEND kuhakikisha kuwa wakati mkitekeleza mradi huu wa bomba la mafuta katika Mkoa wetu wa Shinyanga, mnawashirikisha wananchi ili kulinda usalama wa afya zao na mali zao lakini pamoja na yote kuepukana na migogoro au ajali ambazo zitajitokeza katika utekelezaji wa mradi wenu”, amesema RC Macha.

Aidha RC Macha amewapongeza wasimamizi wa mradi wa EACOP na Shirika la AMEND kwa namna ambavyo wanashirikisha wananchi kuanzia katika hatua ya awali kabisa kupitia vikao na mikutano jambo ambalo limepekea kwa sasa wananchi kufahamu kila kitu kuhusu mradi huu tofauti na wakandarasi wengine ambao wamekuwa hawashirikishi wananchi.

Kwa upande wake Meneja wa Mradi kutoka Shirika la AMEND Bi. Dilys Mneney amesema wameanza kutoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi na waendesha pikipiki katika maeneo ya mradi ili kuwasaidia EACOP hatua ya kuchukua endapo ajali ikitokea huku tathmini imekuwa ikifanyika pia ili kufahamu miundombinu ambayo inatumiwa na magari ya EACOP.

Akielezea hali ya usalama barabarani, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga SACP Janeth Magomi amesema kwa sasa hali ya usalama ni nzuri ukilinganisha na miaka iliyopita kwani wanafanya kila wanaloweza na kutumia vifaa vya kisasa kubaini wanaovunja sheria za barabarani ili kuzuia ongezeko la ajali katika maeneo ambayo yamekuwa yakikumbwa na ajali mara kwa mara.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa