• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri kutumia mfumo maalumu kuajiri Watumishi wa Afya

Posted on: June 12th, 2018

Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini zimetakiwa kutumia mfumo maalumu wa kuajiri na kusambaza watumishi wa kada ya Afya kulingana na uzito wa kazi katika vituo vya Afya na Zahanati.

Katibu Tawala Msaidizi Huduma za Afya katika Sekretarieti ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. Rashid Mfaume ametoa wito huo, akifungua kikao kazi cha kuwasilisha matokeo ya zoezi la kubaini mahitaji ya watumishi kwa kutumia mfumo wa WISN plus POA kwa Mikoa ya Mara na Manyara yaliyofanyika Mkoani Shinyanga mapema wiki hii.

Mfumo huo wa WISN plus POA hutumika kukokotoa mahitaji ya watumishi kwa kila kada katika kituo cha kutolea huduma za Afya.

Kwa sasa mfumo huu unatumika kwa ajili ya Vituo vya afya na Zahanati tu, kwa kada mbalimbali zilizopo katika ngazi hizo za utoaji huduma ambazo ni waganga, matabibu, maafisa wauguzi na wauguzi.

Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mradi wa uimarishaji mifumo ya Sekta ya Umma nchini (PS3), pamoja na Taasisi ya Touch foundation walifanikiwa kutengeneza toleo jipya lililorahisishwa la mfumo huo wa WISN plus POA unaouzingatia uzito wa kazi katika vituo vya kutolea huduma ambapo hivyo kupunguza changamoto ya gharama za kutembelea vituo kwa ajili ya kukusanya taarifa kama ilivyofanyika hapo awali.

Kwa upande wake mwakilishi kutoka OR- TAMISEMI, Bw. Elias Magere amesema Halmashauri zote 185 nchini zimeshapata mafunzo ya kutumia mfumo huu ambapo Maafisa Utumishi, Waganga Wakuu wa Mikoa, Makatibu wa Afya na Waratibu wa MTUHA kwa ngazi za Mikoa na Halmashauri walishiriki.

Afisa TEHAMA wa OR – TAMISEMI Bw. Baraka Emmanuel amesema kuwa, mfumo huu unalenga kuimarisha rasilimali watu katika Sekta ya Afya na pia Maafisa Utumishi wataweza kujua mahitaji halisi ya watumishi na kutoa taarifa za watumishi wapya watakaoripoti kwenye vituo vya Afya kwa urahisi.

Bw. Baraka ameongeza kuwa, mfumo utarahisisha mchakato wa ajira za Afya na Serikali kupeleka watumishi wengine haraka zaidi kwenye vituo iwapo watumishi waliopangiwa hawataripoti kwa wakati.

Naye Afisa Rasilimali watu kutoka Mradi wa PS3 Bi. Scholastica Komba amesema kuwa mfumo wa WISN plus POA ni muhimu sana kwa kada ya Afya kwani wananchi watapata huduma za Afya inavyostahili kutokana na uwepo wa watumishi wa kutosha kulingana na mahitaji.

Kikao kazi hicho kilichofanyika kwa makundi kuanzia tarehe 04 hadi 12 Juni, mwaka huu katika ukumbi wa Liga Hotel Mkoani Shinyanga kimejumuisha Mikoa ya Shinyanga, Singida, Simiyu, Mara, Manyara na Mwanza.

Baadhi ya wawezeshaji wa kikao kazi kilichofanyika Mkoani Shinyanga 

wakiwa katika picha ya pamoja kutoka kushoto ni Bw. Haruni Mwakilasa

 mwakilishi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, 

Jinsia, Wazee na Watoto, Bw. Elias Magere wa OR - TAMISEMI, 

Bi. Scholastica Komba wa PS3 na Bw. Baraka Emmanuel kutoka OR - TAMISEMI.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa