• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

IWE MVUA AU JUA LAZIMA WANANCHI TUWAFIKIE - DC MBONI MHITA

Posted on: April 8th, 2024

Na. Paul Kasembo - Msalala, Kahama.

MKUU wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita ameendelea na ziara yake ya kupokea, kusikiliza na kutatua kero za wananchi maeneo mbalimbali ya Wilaya bila kujali vikwazo anavyokutana navyo kama vile mvua kubwa inayopelekea kuharibika kwa miundombinu ya barabara, hku akisisitiza kuwa "Iwe mvua, iwe jua lazima kuwafikia wananchi walipo na kutatuankero zao".

Aidha, Mhe Mboni amesema kuwa, katika kuendelea kutafsiri maono ya Mhe. Rais na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni muhimu zaidi kuwapa kipaumbele wananchi, maslahi yao ili kuwaletea maendeleo ya kweli.

Katika utekelezaji wa zoezi hili, Mhe. Mboni amepokea kero zinazowakumba wamiliki wa Kampuni za uchimbaji wa madini nankuzipatia ufumbuzi na baadhi ya kero amemuelekeza Afisa Madini Mkazi (RMO) kufanya kikao na wadau wote wanaojihusisha na uchimbaji wa madini na kujadili changamoto hizo kwa pamoja na kuzitafutia ufumbuzi.

Aidha meendelea kuwaelekeza na kuwasizitiza Wadau wa uchimbaji wa madini kuwa na mahusiano mazuri na jamii inayozunguka migodi yao na kuzingatia kuwa, jamii inanufaika ikiwa ni pamoja na ajira ndogondogo (casual labour) ndani ya migodi yao.

Kando na hayo, DC Mnoni, amewaelekeza wadau wa uchimbaji wa madini kuzingatia utunzaji wa mazingira na kuwa na Mpango Mkakati wa muda mrefu wa Utunzaji wa Mazingira (Environmental Management Plan) na kuzikumbusha Kampuni za uchimbaji wa madini kuimarisha kushirikiana na Halmashauri pamoja na Jamii katika kutekeleza Miradi ya CSR ili kutekeleza miradi ya vipaumbele na kuwa na miradi inayotokana na sauti za wananchi.

Mwisho DC Mnoni amemwelekeza Mkurugenzi wa Kampuni ya uchimbaji ya SOJEM kulipa kodi ya Serikali anayodaiwa ya Dollar 3,500 ambapo Mkurugenzi huyu ameahidi kulipa ndani ya siku 14 zijazo kuanzia sasa.


MATUKIO KATIKA PICHA

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa