• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA UTEKELEZAJI MRADI WA UMWAGILIAJI NYIDA, SHINYANGA.

Posted on: March 13th, 2025

Repost from @nirc_tz

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Deodatus Mwanyika (MB) imeridhishwa na utekelezaji wa miradi inayofanywa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), ikiwemo ujenzi wa Mradi wa Bwawa la Umwagiliaji la Nyida uliopo Halmashauri ya Manispaa mkoani Shinyanga.

Kamati hiyo imetembelea mradi huu Machi 13, 2025 ili kujionea utekelezaji wa mradi wa Bwawa la Umwagiliaji la Nyida unaogharimu Tzs. Bilioni 13.6 utakaonufaisha eneo la Umwagiliaji la hekta 800 kwa Nyida na hekta 1,500 kwa Lyamalagwa na zaidi  ya wakulima 4,5000 watanufaika, na hivyo kuakisi kinachofanywa na Tume kinaendana na thamani ya fedha inayowekezwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika miradi ya umwagiliaji nchini.

Akizungumza katika ziara fupi ya kukagua miradi hiyo mkoani Shinyanga, Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Deodatus Mwanyika, amesema kamati inaridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo na kwamba thamani ya fedha inaonekana, huku akiongeza kuwa anaamini malipo yaliyobaki ya kiasi cha Tzs Bilioni 5.6 ili kukamilisha mradi huo unaogharimu Tzs. Bilioni Sh13. 6 yatafanyika kwa wakati ili wananchi waone na kufurahia matunda yake.

“Kamati inaridhishwa kwa kiasi kikubwa na utekelezaji w mradi huu hata kwa macho ukiangalia ujenzi wa ofisi, bwawa na miundombinu mingine inaridhisha na Tzs. Bilioni 8 zilizoanza kufanyiwa uwekezaji zimetumika ipasavyo na zinaonekana, hivyo tunaamini kuwa malipo yaliyobaki kukamilisha mradi huu yatafanyika kwa wakati ili wananchi waweze kuona na kufurahia matunda ya mradi huu, " amesema Mhe. Deodatus.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, alisema mkoa unaipongeza Wizara na NIRC kwa kazi kubwa inayofanyika katika ya miradi ya Umwagiliaji kwani mara kwa mara ametembelea mradi huu na amejionea Tume inafanya mambo makubwa chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Waziri wa Kilimo, Mhe.Hussein Bashe ameahidi atafanya uwekezaji hapa kwa kujenga mashine na ghala hivyo wakulima wa mpunga watauza mchele na kunufaika zaidi kiuchumi.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa