• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MAKANA AZIELEKEZA SHULE ZOTE NA VYUO MKOA WA SHINYANGA KUANZISHA KLABU ZA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Posted on: October 23rd, 2023

Na. Shinyanga RS.

Muwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Ibrahim M. Makana amezielekeza shule na vyuo vyote Mkoa wa Shinyanga kuanzisha Klabu za Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya mwanafunzi wenye maadili mema na kuongeza ufaulu katika masomo yao

Makana ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Menejimenti ya Ufuatiliaji na Ukaguzi Mkoa wa Shinyanga aliyemuwakilisha Katibu Tawala Mkoa Pro. Siza Tumbo pamoja na mambo mengine aliwaeleza washiriki wa mafunzo kuwa, uwepo wa klabu hizi kunakwenda kuimarisha uwezo wa walimu  katika kusimamia klabu hizi ngazi ya shule na vyuo jambo ambalo litapelekea kuwa na wanafunzi ambao ni raia wema, viongozi bora na wazalendo kwa taifa letu.

"Nazielekeza shule zote na vyuo vyote hapa mkoani shinyanga kuhakikisha zinaanzisha klabu hizi za maadili ya uongozi wa umma kwakuwa kuna uhusiano mkubwa sana kati yake na ufaulu wa masomo ya wanafunzi", alisema Makana.

Kwa Upande wake Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Magharibi Ndg. Gerald Mwaitebele amesema kuanzishwa kwa klabu hizi zitasaidia kuwajengea wanafunzi kujua maadili yanayopaswa kuzingatiwa katika ujenzi wa Taifa letu pamoja na kuwa wamzalendo wa kweli.

Kwakuwa ili Taifa liweza kupata viongozi wenye maadili na kizazi chenye uadilifu, ni muhimu walimu kutumia njia vikao vya wazazi mashuleni ili kufikisha ujumbe wa mambo ya maadili kupitia klabu walizozianzisha.

Aidha, Ndg. Mwaitebele ameeleza sifa za mwalimu anayefaa kuwa mlezi katika klabu za maadili ikiwemo Mwadilifu, Mwaminifu, Muwazi,Mzalendo, Mchapakazi na anayekubalika kimaadili na wanafunzi.

Mwaitebele na timu yake ya maadili wwakiwa na waratibu wametembelea shule na vyuo mbalimbali ambazo tayari zimeanzisha klabu hizi za maadili ambapo wamesikiliza ngonjera, mashairi, maigizo na nyimbo kutoka kwa wanafunzi zikiwa na lengo la  kuhamasisha na kukuza  maadili ya umma na kwa watu wote.

Ndg. Gerald Mwaitebele Katibu Msaidizi OR, Sekretalieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Magharibi

Ndg. Onesmo Msalangi Afisa Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Magharibi

Mwl. Bakari Kasinyo (aliyesimama) ambaye Mratibu wa Klabu za Maadili ya Viongozi wa Umma Mkoa wa Shinyanga

Picha ikionesha walimu wa klabu za maadili wakiwa katika mafunzo


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa