• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MAMLAKA ZA MAJI NA TAASISI LIPENI MADENI YENU KASHWASA

Posted on: May 22nd, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ameziagiza Mamlaka na Taasisi zote zinazodaiwa na KASHWASA kulipa madeni yao yote kwa wakati na kwa muda waliokubaliana ili kuiwezesha kutoa huduma bora na stahiki kwa wananchi wa Mikoa hii sita (6) inayoihudumia huku akitoa wito pia kwa wananchi kulipa Ankara zao kwa wakati zaidi na kuepuka usumbufu pindi wanapokatiwa huduma ya maji.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 22 Mei, 2024 alipokuwa akifungua Kikao cha kupata taarifa ya Mpango Biashara wa KASHWASA kwa mwaka 2024/2025 na 2026/2027 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo kwenye ofisi ya KASHWASA na kuhudhuriwa na viongozi wa Bodi, Wakurugenzi wa Mamlaka za Maji, Menejimenti ya RUWASA, Menejimenti ya KASHWASA, na Makatibu kutoka Vyombo vya Watoa Huduma za Maji Ngazi ya Jamii katika maeneo yote yanayohudumiwa na Ziwa Victoria.

"Nizielekeze Mamlaka za Maji na Taasisi zote zinazodaiwa fedha na KASHWASA kuhakikisha mnalipa madeni yote kwa wakati na kwa muda mliokubaliana ili kuwaezesha maboresho katika utoaji wa huduma na kuimarisha uzalishaji", amesema RC Macha.

Kando na wito huu, RC Macha amewataka wananchi kuwa na utaratibu wa kuguatilia na kufahamu kama kuna namna yoyote ile inayopelekea ongezeko la ankara/bili zao kupitia mifumo ya mabomba katika nyumba zao ili kuepuka kuzilaumu Mamlaka za Maji kuwa zinawaongezea gharama katika mara ankara zinapokuwa zimetolewa.

Aidha amezitaka Mamlaka za Maji kudhibiti na kupunguza kama siyo kuondoa kabisa changamoto ya upotevu wa maji katika uzalishaji au usambazaji ambapo kwa sasa inakadiliwa kufikia asilimia 21 kiasi ambacho amekitaja kuwa ni kikubwa sana kwa dhana ya upotevu.

Akitoa taarifa kikaoni Mkurugenzi Mtendaji wa KASHWASA Mha. Patrick Nzamba amesma kuwa uwepo wa Kikao hiki leo ni utekelezaji wa Sera ya Maji ya mwaka 2002 kwamba uendeshaji wa huduma ya maji vijijini utafanywa kwa zingatia Mpango Biashara ulioandaliwa na Mamlaka na kutekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu (3) kama ambavyo leo kikao kimeanza kujadili kwa miaka mitatu ijayo.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa