• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MHA. JUMBE AMEUCHUKUA KWA UZITO MCHEZO KATI YA STAND UTD NA GEITA GOLD FC - JACKLINE

Posted on: January 10th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

Mratibu wa safari ya mashabiki wa Stand United Football Club (Chama la Wana) ya Shinyanga Bi. Jackline Buhali watakaokwenda kuishangilia katika mchezo  dhidi ya Geita Gold FC utakaochezwa January 12, 2025  amesema kuwa Mhandisi James Jumbe kama mdau wa michezo anauchukulia kwa uzito mkubwa mchezo huo na ndiyo sababu ameamua kuwalipia gharama za kwenda na kurudi Geita mashabiki zaidi ya 200.

Bi. Jackline ameyasema haya Januari 10, 2025 alipokuwa akizungumza na Wandishishi wa Habari  mkoani Shinyanga juu ya uwepo wa ufadhiri huu kwa mashabiki na umuhimu wa mchezo huo kwa Mha. Jumbe mchezo ambao utakaofanyika mkoani Geita 12 Januari, 2025 huku donge nono la Sh, 3 Milioni likitangazwa kwa ushindi wa timu na motisha kwa ya Tzs. Laki mbili kwa kila bao litakalofungwa.

"Mhandisi Jumbe ameuchukulia kwa uzito mkubwa mchezo wa Championship  kati ya Stand United FC (Chama la Wana) na Geita Gold FC utakaochezwa Januari 10, 2025 Uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita na ndiyo maana ameamua kuwalipia gharama ya kwenda na kurudi mashabiki zaidi ya 200 watakaokwenda kuishangilia timu hiyo," amesema Bi. Jackline.

Hii ni sehemu ya kurejesha heshima ya Mkoa wa Shinyanga katika soka kwa kusapoti timu hii inayodhaminiwa na Makampuni ya Jambo Group sanjari na kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuendeleza Sekta michezo nchini.

Kwa uapnde wake Afisa Habari wa timu ya Stand United FC ndg. Ramadhani Zoro pamoja na shukrani nyingi kwa Mhandisi Jumbe,  amesema wachezaji wote wana afya njema, ari ya kucheza na nguvu ya kutosha na kwamba mashabiki wote waendelee kuisapoti timu hiyo na watarajie matokeo ya ushindi kuelekea mchezo wao dhidi ya Geita Gold FC wakiwa ugenini.

Stand United FC ya mkoani Shinyanga inayocheza Ligi ya Championship kwa msimu wa 2024/2025  mpaka sasa imecheza jumla ya michezo 14 na kukusanya alama 29 na inatazamwa kama moja ya timu yenye kuleta matumaini ili msimu ujao Mkoa uweze kupata timu ya Ligi Kuu kama ilivyokuwa miaka kadhaa iliyopita ambapo mkoa huu ulikuwa na timu za Mwadui FC na Stand United FC.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa