• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MHE. CHEREHANI AONGOZA HARAMBEE

Posted on: January 12th, 2025

MHE. CHEREHANI AONGOZA HARAMBEE

USHETU.

Zaidi ya Shilingi Milioni 50 zimekusanywa katika harambee iliyofanyika kwa ajili ya Ujenzi wa Bweni la Wasichana katika Shule ya Sekondari Chona iliyopo katika Kata ya Chona Halmashauri ya Ushetu Wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Fedha hizo zimekusanywa katika hafla  ya kufungua Mwaka  iliyofanyika leo  ambayo imewahusisha wadau mbalimbali wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Emmanuel Cherehani, Diwani wa Kata ya Chona ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa, Mkurugenzi wa Gold FM Bi. Neema Mghen pamoja na wadau wengine ambapo kiasi cha shilingi milioni 25 zimepatikana huku shilingi milioni 25 zikiahidiwa.

Akizungumza katika hafla hiyo Mbunge  Cherehani ameitaka Kamati ya Shule hiyo kusimamia vyema fedha hizo ili ziweze kukamilisha ujenzi huo huku akiwakumbusha wazazi na walezi kuwapeleka shule watoto wao ili waweze kutimiza ndoto zao na kuzisaidia familia zao na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Mwenyekiti  Mabala Mlolwa amesema kukamilika kwa bweni hilo kutamsaidia mtoto wa kike katika kutimiza ndoto zake, huku Mkurugenzi wa Gold FM Bi. Neema Mgheni akiwahimiza Wadau wengine wa Maendeleo kuendelea kujitoa katika sekta ya elimu.

Awali akisoma risala Afisa Mtendaji wa Kata hiyo Masamaki Madaha amesema watoto wa kike wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kutembea zaidi ya kilomita 10 kuifikia shule pamoja na kurubuniwa na kutumbukia kwenye vitendo vya ngono hali inachangia kukatisha masomo yao.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa