• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MHE. RIDHIWANI KIKWETE AWAKARIBISHA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LA MKOA WA SHINYANGA KWENYE MAONESHO YA SABASABA

Posted on: July 5th, 2025

Sabasaba 2025

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Kikwete, ametoa wito kwa wananchi wote wanaotembelea Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutembelea Banda la Mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya kupata huduma, bidhaa na taarifa za fursa mbalimbali zinazopatikana katika Mkoa.

Mhe. Ridhiwani alitoa wito huo alipofanya ziara katika banda hilo lililopo mkabala na Banda la TANESCO, huku akiipongeza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kwa uratibu mzuri, usimamizi makini na ushiriki wa hali ya juu katika maonesho hayo.

Katika ziara hiyo, Waziri Ridhiwani aliambatana na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobas Katambi, ambapo walipata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali ndani yakiwemo yale kutoka Halmashauri zote za Shinyanga.

“Nawapongeza kwa kazi nzuri mliyoifanya katika kuandaa banda hili. Bidhaa mlizozileta, huduma mnazotoa na namna mnavyowasiliana na wafanyabiashara wengine hakika ni ya kiwango cha juu na hii ni fursa nzuri kwa wafanyabiashara kujifunza na kunufaika,” alisema Mhe. Ridhiwani.

Kwa upande wake, Mhe. Patrobas Katambi aliupongeza uongozi wa Mkoa wa Shinyanga pamoja na wafanyabiashara wote walioshiriki kwa juhudi kubwa waliyoonyesha katika kutangaza bidhaa, huduma na fursa za kiuchumi zinazopatikana mkoani humo.

“Ushiriki wenu ni kielelezo cha dhamira ya dhati ya kuutangaza Mkoa wa Shinyanga, ni hatua muhimu katika kujitangaza, kuzitangaza bidhaa na huduma na kukuza uchumi wa ndani na kuongeza ajira kwa vijana,” alisema Mhe. Katambi.

Banda la Mkoa wa Shinyanga linabeba dhima ya kuonesha mafanikio ya Mkoa katika Sekta mbalimbali zikiwemo viwanda vidogo, kilimo, biashara, utalii na huduma za kijamii, kuzitangaza fursa za kiuwekezaji zilizopo na hii ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa sera na mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM APONGEZA USHIRIKI WA MKOA WA SHINYANGA KATIKA MAONESHO YA SABASABA.

    July 06, 2025
  • RC. MBONI ATOA WITO KWA TISEZA KUTANGAZA FURSA KUU YA KONGANI YA UWEKEZAJI BUZWAGI

    July 05, 2025
  • MHE. RIDHIWANI KIKWETE AWAKARIBISHA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LA MKOA WA SHINYANGA KWENYE MAONESHO YA SABASABA

    July 05, 2025
  • KATIBU TAWALA WILAYA YA KAHAMA AWAPONGEZA WASHIRIKI WA MAONESHO YA SABASABA 2025 KUTOKA MKOA WA SHINYANGA

    July 05, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa