• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

NAWAPONGEZA SANA BENKI YA CRDB KWA KUANDAA MASHINDANO HAYA - PROF. TUMBO

Posted on: October 14th, 2023

Na. Shinyanga RS.

KATIBU Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo leo tarehe 14 Oktoba, 2023 amemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme kuwa mgeni rasmi katika mashindano ya mbio za baiskeli zinazoandaliwa na Benki ya CRDB katika uwanja wa Kambarage Manispaa ya Shinyanga ambapo pamoja na kuwapongeza CRDB lakini pia amesema kuwa mashindano haya yamesaidia kuutangaza mkoa pamoja na kufungua zaidi fursa za kiuchumi kwa wananchi na uwekezaji pia.

Prof. Tumbo amesema haya kwenye kilele cha Mbio hizi za Baiskeli za CRDB Shinyanga (Shinyanga CRDB Cycling Rally) mbele ya washiriki wa mbio hizi na wananchi kuwa, uwepo wa mashindano haya si tu kwamba zinatoa fursa kwa wananchi wanaoshiriki kuimarisha na kulinda afya zao, bali washindi wanapata zawadi zinazowahamasisha wao na wengine kuendelea kushiriki na mashindano mengine zaidi.

“Mbio hizi zimetoa fursa ya kuutangaza mkoa wetu pamoja na kufungua fursa za kiuchumi kwa wananchi na wafanyabiashara. Kadri miaka inavyozidi Kwenda, umaarufu wa mbio hizi unazidi kuongezeka hivyo basi, wakati Benki ya CRDB ikifungua njia, nitumie fursa hii kuziomba pia kampuni nyingine nazo kuangalia namna ya kufungua fursa za mkoa wetu jambo litakalosaidia kuboresha maisha ya wananchi,” alisema Prof. Tumbo.

Awali kulitanguliwa na shughuli za kijamii ikiwemo kuchangia damu ambapo zaidi ya chupa 500 za damu salama zilikusanywa kwa ajili ya wagonjwa wenye uhitaji wanaotibiwa katika hospitali na vituo vya afya mkoani humu na nchini kote kwa ujumla.

Kwa upande wake Meneja wa CRDB Tawi la Shinyanga Luther Mneney akiongea kwa niaba ya Meneja wa Benki ya CRDB kanda ya Magharibi, Jumanne Wagana amesema mbio hizo hufanyika kila mwaka siku ya kumbukumbu ya baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere, ambaye alipenda kila mwananchi kuwa huru kiuchumi kwa kujituma kufanya kazi kulingana na fursa zilizopo kwenye eneo alilopo.

Luther amesema Benki ya CRDB ni mdau mkubwa wa michezo nchini kutokana na imani kubwa kwamba inajenga ushirikiano, mshikamano, na kuwaleta watu pamoja hivyo kuwa rahisi kuleta maendeleo katika jamii.


HABARI PICHA




Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa