• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

NIWAOMBE TWENDE KUZISOMA VIZURI SHERIA ZA OFISI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA - SHIJA

Posted on: October 22nd, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MWEZESHAJI kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vga Siasa Tanzania ndg. Frank Shija amewaomba Viongozi wa Vyama vya Siasa wilayani Shinyanga kwenda kuzisoma vizuri Sheria zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Tanzania @orpptanzania kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 huku akiwakumbusha kutanguliza uzalendo pia katika utekelezaji wa majukumu yao hasa wanapoelekea kuanza kampeni.

Shija ameyasema haya leo tarehe 22 Oktoba, 2024 alipokuwa akizungumza na Viongozi katika Wilaya ya Shinyanga inayounganisha Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga na Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine amewapatia wajumbe vitabu vya Sheria hizo na amewaomba ushirikiano wao kwa kipindi ambacho watakuwa hapa mkoani Shinyanga.

Akifungua mafunzo haya, Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga amewaomba kwenda kufanya kampeni na kutangaza Sera za Vyama vyao kwa ustaarabu, kuwa wazelendo, kupendana, umoja, kushirikiana na kuacha kutuhumiana kwa mambo yasiyokuwa na ukweli kwani kuna maisha yataendelea baada ya uchaguzi.

Aidha, wajumbe wa mafunzo haya wamekiri kupokea vitabu vyenye kuelezea Sheria hizi huku wakiahidi kwenda kuzipitia kwa umakini huku wakiiomba Ofisi ya Msajili kuwa karibu nao zaidi ukizingatia kuwa kipindi hiki ni cha kuelekea kampeni kuanza kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambapo wamesema huwa kuna sintofahamu kadhaa huwa zinajitokeza kwa hiyo uwepo wa wawakilishi hawa kutasaidia sana.

Kando nao, Msimamizi wa Uchaguzi katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Mwl. Alexius Kagunze na Dkt. Kalekwa Kasanga wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa nyakati tofauti wamewashukuru sana viongozi wa Vyama vya Siasa wilayani Shinyanga kwa namna ambavyo wamekuwa wakiwapatia ushirikiano wakati wote

Novemba 27, 2024 ni siku ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ambapo wananchi watapata nafasi ya kuchagua viongozi wao wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji ambao watawahudumia kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa