• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

PFOR. SIZA TUMBO AKABIDHI OFISI KWA KATIBU TAWALA MKOA WA SHINYANGA CP. SALUM HAMDUNI

Posted on: August 22nd, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

ALIYEKUWA KATIBU Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza D. Tumbo akabidhi ofisi kwa Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Rashid Hamduni ambaye ameteuliwa hivi karibuni na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan huku akiwaomba watumishi wote, wadau na wananchi wote Mkoa wa Shinyanga kumpatia ushirikiano RAS Hamduni kama ambavyo walikuwa wakimpatia ili aweze kutimiza majukumu yake kikamilifu.

Haya yamesemwa na leo tarehe 22 Agosti, 2024 wakati akikabidhi ofisi kwenye hafla iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ambapo viongozi mbalimbali wamehudhuria wakiwemo na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Julius Mtatiro (Wakili).

Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude, Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita, Kamati za Usalama, viongozi wa Chama Cha Mapinduzu, Wakuu wa Taasisi za Serikali na zisizo za Serikali,viongozi wa Kimila, Kamati ya Maridhiano, viongozi wa wachimbaji wa madini, wadau wa maendeleo na watumishi wote.

"Nichukue nafasi hii kuwashukuru nyote kwa ushirikiano wenu mlionipatia wakati wote katika kutekeleza majukumu yangu, na sasa niwaombe rasmi ushirikiano huo huo muendeleze kumpatia RAS CP. Hamduni ili aweze kutekeleza vema wajibu na majukumu yake hapa mkoani Shinyanga," amesema Prof. Siza Tumbo.

Kwa upande wake CP. Hamduni amemshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kumuwezesha Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kumteua kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga na kwamba amekuja kuwatumikia Wanashinyanga kama Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga na siyo katika nyadhifa nyinginezo huku akiwaomba ushirikiano wakati wote ili aweze kutekeleza majukumu yake.

Kipekee, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amempongeza sana Prof. Siza Tumbo kwa kazi nzuri na njema sana aliyoifanya hapa Mkoa wa Shinyanga, amekuwa Mwalimu wakati wote wa utumishi wake kwa watumishi wengine wote akiwemo yeye mwenyewe RC Macha. 

Makabidhiano haya yanafanyika kufuatia mabadiliko ya aliyekuwe RAS Shinyanga ambaye amerejeshwa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA)

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa