• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Profesa Ndalichako awa mbogo kasi ndogo ya Mkandarasi wa ujenzi Chuo cha Ualimu Shinyanga, ampa mwezi mmoja kukamilisha kazi ya bil. 2.7

Posted on: October 5th, 2018

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Profesa Joyce Ndalichako amemtaka Mkandarasi wa ujenzi na ukarabati katika chuo cha ualimu Shinyanga kampuni ya “Afrique Co. Ltd” kuhakikisha ndani ya mwezi mmoja anakamilisha kazi zote anazotakiwa kutekeleza kwani ameshalipwa karibu fedha yote lakini kasi yake hairidhishi.

Prof. Ndalichako pia amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kumuondoa mara moja Mkuu wa chuo cha Ualimu Shinyanga (Shycom) na kumtaka Mkurugenzi wa Taasisi ya kupambana na kuzuia Rushwa TAKUKURU kuanza kufanya uchunguzi wa mwenendo wa manunuzi katika mradi wa upanuzi na ukarabati wa majengo katika chuo hicho.

Ndalichako ametoa agizo hilo mapema leo tarehe 05 Oktoba, 2018 alipotembelea chuo hicho cha Ualimu kukagua maendeleo ya mradi wa upanuzi na ukarabati wa majengo unaogharimu Serikali sh. Bilioni 9.4 na kuzungumza na wanafunzi pamoja na wakufunzi.

Amesema amesikitishwa na kushangazwa na kasi ndogo ya kiwango cha ujenzi ambapo Mkandarasi huyo ameshalipa jumla ya sh. bil. 2.7 pamoja na kitendo cha Mkuu wa Chuo kumsifia kuwa anafanya vizuri wakati Mkandarasi mshauri wa mradi ambaye ni Makamu Mkuu wa Chuo kikuu cha Ardhi Profesa Evaristo Liwa amesema hakuridhika na mwenendo wa mkandarasi huyo tangu mwanzo.

Kwa mujibu wa taarifa ya mshauri huyo, mkandarasi alishapewa onyo mara tatu na alishauri Wizara ivunje  naye mkataba lakini cha ajabu Wizara imemlipa tena mkandarasi huyo sh. bilioni 244 tarehe 02 Oktoba ambapo Ndalichako amesema, maafisa Elimu pia wa Wizara yake wachunguzwe.

Aidha amemtaka pia mkandarasi wa pili katika mradi huo kampuni ya Masasi Construction kukamilisha kazi zake maramoja kwani na yeye mkataba umeisha muda wake.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko ameahidi atafuatilia na kumsimamia mkandarasi kuhakikisha kazi zote zinakamilika ndani ya mwezi mmoja na kumpa taarifa Waziri.

Mradi huo wa ujenzi, upanuzi na ukarabati wa majengo unaotekelezwa na Serikali katika vyuo vinne vya ualimu nchini nzima ikiwemo chuo cha Ualimu Shinyanga, una thamani ya zaidi ya sh. Bilioni 36.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa