• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN ATOA MKONO WA PASAKA KWA MAKAO YA WATOTO YATIMA NA MAKAZI YA WAZEE NA WENYE MAHITAJI MAALUMU.

Posted on: April 16th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY DC.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa mkono wa Sikukuu ya Pasaka kwa Makazi ya Wazee na Wenye Mahitaji Maalumu Usanda yaliyopo Halmasahuri ya Wilaya ya Shinyanga na Makao ya Watoto Yatima na Wanaoishi katika Mazingira Hatarishi ya Beauty for Ashes yaliyopo Kitangiri Manispaa ya Shinyanga ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Sikukuu pamoja nao..

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi hizo, Bi. Lydia Kwesigabo ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Shinyanga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha alisema kuwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaagiza kupeleka zawadi hizo kwa wazee na watoto hao ili kuwashika mkono katika kusherehekea Sikukuu na kwamba anatambua, anathamni, anaheshimu na anawajali sana wao kama sehemu ya jamii na kwamba wao pia kama walivyo watoto na wazee wengine wanazo haki na stahiki sawa.

"Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, mimi pamoja na watumishi wenzangu tumekuja hapa kuleta zawadi zilizotolewa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenu ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Sikukuu ya Pasaka pamoja naye ambapo ametupatia vitu mbalimbali ikiwemo Mchele, Mafuta ya Kupikia, mboga (mbuzi), Sharubati (juice), sabuni,mafuta ya kujipaka, wipers. pampers na maziwa kwa watoto hawa wachanga hivi vyote tumeagizwa tuwaletee na pia ametoa salamu zake kwenu kuwa anawapenda sana na yupo pamoja nanyi," alisema Lydia.

Huu ni muendelezo wa utoaji zawadi kwa Makao na Makazi [9) mbalimbali hapa mkoani Shinyanga, ambapo awamu ya kwanza zawadi zilitolewa ikiwa ni wakati wa kuelekea Sikukuu ya Eid Al - Fitr na sasa ni kuelekea Sikukuu ya Pasaka.



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa