• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RAS CP. HAMDUNI AKABIDHI VITENDEA KAZI ILI KUBORESHA UTOAJI HUDUMA ZA AFYA MKOA WA SHINYANGA

Posted on: January 2nd, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

KATIBU Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Hamduni kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amekabidhi vitendea kazi ili kuweza kuboresha utoaji wa huduma hapa mkoani Shinyanga huku akisisitiza utunzaji wa vitendea kazi hivi ambavyo Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais TAMISEMI imetoa magari manne (4) ya wagonjwa (Ambulance), gari la chanjo moja (1) na pikipiki kumi (10).

RAS CP. Hamduni amekabidhi leo tarehe 2 Januari 2025 kwa Faustine Mlyutu ambaye ni muwakilishi wa Mganga Mkuu Mkoa wa Shinyanga Daktari Yudas Ndungile pamoja na Waganga Wakuu wa Halmashauri na kumshukuru sana Mne. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuboresha utoaji huduma mbalimbali katika jamii ikiwemo afya.

"Kwa niaba ya Serikali ninawakabidhi vitendea kazi hivi ikiwa ni magari 4 ya kubebea wagonjwa (Ambulance) kwa Halmashauri ya Shinyanga DC, Kishapu DC, Msalala DC na Ushetu DC, gari 1 la Mkoa kwa ajili ya kusambaza Chanjo na pikipiki 10 kwa Kahama MC 1, Msalala DC 2, Shinyanga DC 2, Kishapu DC 1, Ushetu DC 1 na Shinyanga MC 1. Aidha nitumie nafasi hii kutaka kwenda kuhakikisha vifaa hivi vinatunzwa kwa maslahi makubwa ya wananchi wetu na Taifa kwa ujumla," amesema RAS CP. Hamduni.

Huu ni muendelezo wa dhamira ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuhakikisha inaboresha, kulinda na kuimarisha afya za wananchi wake sanjari na kusimamia na kutafsiri maono ya Mhe. Rais kwa vitendo kupitia Sekta mbalimbali ambapo Mkoa wa Shinyanga takribani Vijiji vyote 506 vinavyounda Mkoa vimefikiwa na miradi ya maendeleo.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa