• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AKABIDHI ZAWADI KWA WAZEE WASIOJIWEZA - KOLANDOTO

Posted on: April 11th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ametembea na kukabidhi zawadi ya chakula, vinywaji, sabuni, mafuta na chumvi kwa Kituo cha Kulelea Wazee Wasiojiweza kilichopo Kolandoto Manispaa ya Shinyanga huku akiwahakikishia wazee hawa kuwa Serikali ipo pamoja nao, haina ubaguzi wa aina yoyote na maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kwamba kila mmoja ataishi kwa furaha na amani zaidi nchini mwao.

RC Macha ameyamesema haya wakati akizungumza na wazee hawa ambao kwa sehemu kubwani kundi maalum wapatao 18 ambapo pamoja na mambo mengine amemtaka Mhandisi wa Manispaa ya Shinyanga kwenda kufanya tathimini ya eneo, kutengeneza mchoro wa jengo la kisasa lenye vyumba 20 ili Serikali iweze kuwajengea wazee hawa ikiwa ni sehemu ya kuboresha makazi yao.

"Nawaagiza wataalam wa Manispaa ya Shinyanga kufika hapa Kituo cha Kulelea Wazee - Kolandoto ili kufanya tathimini na kuchora ramani ya jengo la vyumba 20 ili Serikali iweze kuwajengea nakuboresha makazi yao," amesema RC Macha.

Kituo cha Wazee Kolandoto kilianzishwa rasmi mwaka 1977 ambapo kimekuwa kikihudumiwa na Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo Jamii, Jinsia, Wanawake na wenye Mahitaji Maalum na kwa sasa walengwa wote waliopo hapa wanapata chakula kuazia asubuhi, mchana na usiku.

Pia wamepatiwa Bima ya afya ambapo wanapata huduma ya matibabu bure wakati wote na kwa msisitizo wa RC Macha kuanzia sasa Serikali ya Mkoa wa Shinyanga itakitazama kwa ukaribu zaidi Kituo hiki.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa