Na. Paul Kasembo, SHY RS.
MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amemkabidhi Kitimwendo na Tzs. 300,000/= (Laki tatu) mtoto Ester Maiko ambaye ni mwenye ulemavu wa viungo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Mhe. Patrobas Katambi Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini pamoja na Mhe. Christina Mzava ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga wakati wa Kongamano la Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA) wakiadhimisha Siku ya Wanawake na Wanawake wenye ulemavu, ili kiweze kumsaidia mtoto na mzazi wake aweze kufanya biashara ndogondogo ambayo itamuwezesha kujikimu kwa namna moja au nyingine.
Akizungumza baada ya kukabidhi msaada huo, RC Macha alimshukuru sana Mhe. Katambi na Mhe. Christina kwa namna ambavyo waliweza kuguswa, kujitolea na kumsaidia mtoto Ester na mzazi wake katika uhitaji wao huku akiwapongeza (SMAUJATA) ngazi zote kwa kuweza kufuatilia, kuibua na kusimamia mambo mbalimbali likiwemo hili la mtoto Ester pamoja na mambo yote yanayohusu mapambano dhidi ya ukatili wa aina yoyote ile kwa jamii zetu.
"Kwa dhati kabisa, ninamshukuru sana Mhe. Katambi kwa kutoa kitimwendo na Mhe. Christina kwa kutoa fedha Tzs. 300,000/= (laki tatu) kwa mzazi wa ambazo zitamsaidia kufanya shughuli ndogondogo za kujikwamua kimaisha changamoto ambayo iliibuliwa na SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga katika Kongamano la Siku ya Wanawake na Wanawake wenye Ulemavu, na kipekee pia niwapongeze SMAUJATA kwa kazi nzuri mnayoendelea nayo ya kuihudumia, kuipambania na kuisogelea jamii yetu," alisema RC Macha.
Ikumbukwe kwamba, mnamo tarehe 1 Machi, 2025 kulifanyika Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake na Wanawake wenye Ulemavu Mkoa wa Shinyanga katika ukumbi wa Lyakale Manispaa ya Shinyanga ambapo uwepo wa mtoto Ester na changamoto yake iliyokuwa na uhitaji wa kitimwendo na msaada zaidi iliyoibuliwa na SMAUJATA kwa lengo la kumsaidia na ndipo ahadi za Waheshimiwa Wabunge zilitolewa na leo zimetekelezwa kwa vitendo.
Boma Street, Mwanza Road
Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga
Simu: +255 28 2762222
Simu ya Mkononi:
Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz
Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa