• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA APOKEA NYARAKA ZINAZOBEBA KERO ZA WANAKAHAMA

Posted on: October 10th, 2024

Na.Paul Kasembo, KAHAMA.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe.Anamringi Macha amepokea Nyaraka kutoka kwa Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Taifa Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi zilizobeba kero za wananchi wa Wilaya ya Kahama na kuahidi kuzifanyia kazi huku akiwaomba kuwa watulivu wakisubiri kero zao zitatuliwe.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 10 Oktoba, 2024 baada Balozi Dkt. Nchimbi kupokea kero kutoka kwa wananchi akiwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Majengo na ambao ulilenga kupokea, kusikiliza na kutatua kero zao ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM.

“Nimepokea Nyaraka hizi zilizobeba kero za Wanakahama kutoka kwa Balozi Dkt. Nchimbi na mimi naahidi kuanza kuzifanyia kazi punde baada ya ziara hii kukamilika ili kuhakikisha zinatatuliwa ndani ya muda mfupi, lakini niwaombe Wanakahama muendelee kuwa watulivu kwa kipindi hiki mnachosubiria kero hizi kupatiwa ufumbuzi” amesema RC Macha.

Kando na hilo, suala la uhaba wa umeme liliwasilishwa na Waheshimiwa Wabunge wa Wilaya ya Kahama ambapo wameomba na kupendekeza Wilaya ya Kahama kufanywa kuwa Mkoa wa Ki - TANESCO ili kupunguza changamoto ya umeme.

Kufuatia ombi hili, Dkt. Nchimbi amewasiliana na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati Mhe. Dotto Biteko ambaye alisema kuwa ameshapokea mapendekezo hayo na sasa anayafanyia kazi ili kuhakikisha Wilaya ya Kahama inakuwa Mkoa wa Kitanesko.

Hii ni siku ya pili ya ziara ya Balozi Dkt. Nchimbi hapa mkoani Shinyanga, ambapo kesho atahitimisha hapa wilayani Kahama na baadae atafanya mkutano wa hadhara Manispaa ya Shinyanga kisha Kata ya Maganzo iliyopo wilayani Kishapu.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa