• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AKAGUA UKARABATI WA BWAWA LA MWALUKWA

Posted on: September 29th, 2023

Na. Shinyanga RS

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme ametembelea na kukagua ukarabati wa Bwawa la Mwalukwa lililopo Kata ya Mwalukwa Halmashauri ya Shinyanga na kuagiza ukamilishwaji haraka wa bwawa hili ifikapo Oktoba 15, 2023 ili lianze kunufaisha jamii inayoizunguka pamoja na mifugo huku akionya wananchi kuacha kabisa kufanya shughuli za kibinadamu kandokando mwa bwawa na badala yake watunze vyanzo vya maji eneo hili.

Mhe. Mndeme ameyasema haya wakati alipokuwa akizungumza na uongozi wa Kata ya Mwalukwa, msimamizi wa mradi huu, mafundi wanaojenga bwawa pamoja na wananchi waliokuwa eneo la mradi huu, ambapo pamoja na kupokea taarifa ya ukarabati wa bwawa lakini alimtaka msimamizi wa mradi huu Ndg. Islael Chafumbwe kutoka Wizara ya Maji kuharakisha ukamilishaji wa mradi huu ili kufikia Oktoba 15, 2023 ukarabati uwe umekamilika kama ulivyokusudiwa.

"Niwapongeze wana Kata ya Mwalukwa kwa kupata mradi huu mzuri na wenye tija kwenu ambao unagharimu zaidi ya Milioni 69 fedha kutoka Serikali inayotekelezwa kupitia Wizara ya Maji na Bonde la Maji Bonde la Kati na ambao utanufaisha wakazi zaidi ya elfu 22 na mifugo zaidi yq elfu 13. Lakini nawaagiza kukamilisha mradi huu haraka ili kufikia Oktoba 15, 2023 ukarabati uqe umekamilika tayari kwa matumizi," alisema Mhe. Mndeme.

Bwawa la Mwalukwa linatekelezwa ili kuwezesha upatikanaji wa maji ya uhakika wa wastani wa mifugo nje ya hifadhi ya bwawa kwa kujengewa Mabirika yatakayowezesha mifugo kupata maji ya uhakika wakati wote na kwa matumizi ya nyumbani pia ambapo linatarajiwa kutoa huduma kwa mifugo zaidi ya elfu 13 na watu zaidi ya elfu 22.

Kukamilika kwa bwawa hili kutaongeza ujazo wa lita hadi kufikia 293,651,980 kutoka ujazo wa lita 71,573,020 za awali wakati lilipokuwa na urefu wa mita 2.25 kwa maelezo hayo kunaonesha kutakuwa na ongezeko la ujazo mara nne ya ujazo wa awali hivyo kuimarisha zaidi utoaji huduma kwa wana jamii na mifugo yao.

Hili ni bwawa linalotekelezwa kupitia wataalam wa ndani kwa kuboresha kwa Kingio la maji (TUTA) lenye kimo cha mita 3.50 na urefu wa mita 410, kuboresha tuta linalozuia utoro wa maji wenye upana wa mita 42 ili kuwezesha kuhifadhi maji.

HABARI NA MATUKIO



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa