• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RCC SHINYANGA YAJIRIDHISHA PENDEKEZO LA KUGAWA JIMBO LA UCHAGUZI LA SOLWA KUWA MAJIMBO YA SOLWA NA ITWANGI

Posted on: March 16th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

KAMATI ya Ushauri ya Mkoa wa Shinyanga (RCC) ikiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye ni Mkuu wa Mkoa Mhe. Anamringi Macha imejiridhisha na pendekezo la kugawa Jimbo la Uchaguzi la Solwa kuwa Majimbo ya Sllwa na Itwanhi baada ya kukidhi vigezo vya Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania (INEC) na kwamba Jimbo lina ukubwa wa Kilometa za mraba 4,212 na kiutawala likiwa na Tarafa 3, Kata 26, Vijiji 126 na Vitongoji 856.

Hayo yamejiri wakati wa RCC Maalum ikiyoketi tarehe 15 Machi, 2025 katika Ukumhi wa Mikutano uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, ambapo pamoja na mambo mengi RC Macha aliwaeleza wajumbe kuwa wamefikia hatua hiyo baada ya mchakato huo kupitia hatua zote muhimu ikiwemo kujadiliwa katika Baraza la Waheshimiwa Madiwani na Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Shinyanga (DCC) na sasa RCC.

"Ndugu wajumbe wa RCC tumekutana hapa maalum kujadili pendekezo la kuligaw Jimbo la Uchaguzi la Solwa na kuwa Majimbo mawili yaani Solwa na Itwangi, na hii inakuja baada ya kuwa taratibu zote zimefuatwa na kuzingatiwa ikiwemo kukidhi vigezo vya Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania na kujadiliwa katika Mkutano wa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga na Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Shinyanga na sasa ni zamu yetu RCC," alisema RC Macha.

Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 Jimbo la Solwa lilikuwa na jumla ya wakazi 468,611 ambapo kwa sasa inakadiriwa kuwa na zaidi ya watu 503,167 idadi ambayo ni kubwa sana kwa Mbunge mmoja kuhudumia wananchi kikamilifu.

Kwa taarifa hiyo, Jimbo la Solwa litakuwa na Tarafa moja (01) ya Nindo yenye jumla ya Kata 12 ambazo ni Salawe, Mwenge, Solwa, Mwakitolyo, Lyabukande, Lyamidati, Iselamagazi, Lyabusalu, Pandagichiza, Mwalukwa, Mwantini na Nyamalogoa. Jimbo litakuwa na Vijiji 68 na Vitongoji 478.

Jimbo la Itwangi litakuwa na Tarafa mbili (02) ya Itwangi na Samuye zenye jumla ya Kata 14 ambazo ni Ilola, Didia, Puni, Itwangi, Nyida, Tinde, Nsalala, Usule, Bukene, Imesela,  Mwamala, Samuye, Masengwa na Usanda. Jimbo litakuwa na jumla ya Vijiji 58 na Vitongoji 378.



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa