• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SDC SACCOS IMEJIPANGA KUWANUFAISHA ZAIDI WANACHAMA WAKE - MAZINA.

Posted on: December 7th, 2024

Na. Paul Kasembo, Shy RS.

Mwenyekiti wa Bodi ya  Akiba na Mikopo Wilaya ya Shinyanga (SDC SACCOS) ndg. Epafras Mazina amesema kuwa wamejipanga kikamilifu kuwanufaisha wanachama wake huku akisisitiza kuwa uwepo wa chama hiki umepunguza kadhia kwa kuepuka kuumizwa na mikopo yenye riba kubwa kwani kinawasaidia kukopa na kuboresha maisha yao kwa kuwa kila mwisho wa mwaka kunakuwa na gawio kubwa kwa wanachama wote.

Ameyasema haya tarehe 7 Desemba, 2024 wakati wa mkutano mkuu wa 22 wa mwaka ambao umelenga kufanya tathmini ya maendeleo ya chama  pamoja na kuweka mikakati ya utendaji na utekelezaji kwa kipindi kinachofuata , mkutano ambao umefanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

“Chama hiki kimeendelea kuwasaidia watumishi kwani wanaweza kukopa na kuboresha maisha yao kwa namna moja ama nyingine kwa kuwa kila mwisho wa mwaka kunakuwa na gawio kwa wanachama wote na hii imepunguza kadhia kwa wanachama kwa kiasi kikubwa kwa kuwa hawataumizwa tena na mikopo yenye riba kubwa (kausha damu) kutoka kwenye Mashirika au vikundi vya utoaji mikopo na sasa tutawanufaisha zaidi,” amesema Mazina.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ndg. David Rwazo amewapongeza wanachama kwa ushirikiano mzuri wanaoonyesha lakini pamoja na yote amewataka wanachama kuwa waaminifu kwa kujitahidi kurudisha fedha wanazokopeshwa kwa wakati ili kufanya chama kizidi kusonga mbele na kufanikiwa zaidi.

Ikumbukwe kuwa Chama cha SDC SACCOS kilisajiliwa tarehe 20 Juni, 2006 ili kuunganisha rasilimali fedha za watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa kutoa huduma za akiba na mikopo yenye riba na masharti nafuu zaidi ambapo mpaka sasa kina jumla ya wanachama ambao ni watumishi 2002 kati ya watumishi 2437 katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa