Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Sekta Binafsi zaagizwa kuzingatia Sheria ya kazi

Posted on: May 3rd, 2017

Waajiri wa sekta binafsi Mkoani Shinyanga wameagizwa kuhakikisha wanafuata sheria za kazi ikiwemo kuwapatia mikataba ya kazi ya maandishi watumishi wao pamoja na vitendea kazi ili waweze kufanya kazi katika hali ya usalama.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack wakati wa maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani ambayo kimkoa imefanyika katika uwanja wa Kambarage, Manispaa ya Shinyanga.

Mhe. Telack amemuagiza Katibu Tawala Mkoa kuunda kamati itakayofuatilia utekelezaji wa agizo hilo na kumpatia taarifa.

“Naagiza waajiri wote wa sekta binafsi wiki mbili kuanzia leo kufuata sheria za kazi na
tarehe 15/05/2017 Katibu Tawala Mkoa ataunda kamati ndogo kupitia sekta zote kama wametekeleza maagizo”.

Kuhusu suala la Sekta binafsi kutojali sheria ya Wafanyakazi, Mkoa umekuwa ukiwaagiza wamiliki na watendaji kuzingaria sheria ya ajira na mahusiano kazini mara kwa mara.

 Aidha, Mhe. Telack amesema, Serikali inatekeleza kwa vitendo uwezeshaji katika uanzishaji wa viwanda vikubwa na vidogo hivyo wananchi wote tunapaswa kufanya kazi kwa bidii katika kutoa huduma na bidhaa bora ili kuweza kupata malighafi kwa viwanda vinavyoanzishwa.

“Wafanyakazi bado tunayo fursa ya kujihusisha na kilimo ili kuongeza malighafi,walau kila mfanyakazi awe na ekari moja, hii itapunguza wafanyakazi kuwa wanunuaji tu bali washiriki katika uzalishaji”.

Amesema kuwa, Mkoa umekuwa kivutio cha uwekezaji wa viwanda kutokana na huduma zote muhimu, umeme, maji, amani, utulivu na ukarimu wa wananchi.

Amewataka wafanyakazi na wananchi wote kuwajibika katika kulinda amani na utulivu kwani ni muhimu kwa maendeleo ya Mkoa na nchi kwa ujumla.

Mhe. Mkuu wa Mkoa, ametoa rai kwa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) kuendelea kutoa ushirikiano chanya kwa Serikali na Wafanyakazi. Aidha wafanyakazi watambue kuwa, kuna haki na wajibu hivyo, watumie muda mwingi kutimiza wajibu wao wa kuhudumia wananchi kuliko kulalamika na wachache ambao ni wazito, TUCTA iendelee kuwakumbusha wajibu wao.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa