• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI ITAENDELEA KUWEZESHA WAKULIMA WA PAMBA ANGALAU KILA MMOJA AZALISHE KILO 1,200 KWA MSIMU - RC MACHA

Posted on: January 29th, 2025

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha leo tarehe 29 Januari, 2025 amefanya ziara na kutembelea Vijiji vya Nsunga, Manungu na Bugoshi vilivyopo Kata ya Uyogo Halmashauri ya Ushetu na kuzungumza na wakulima wa zao la Pamba ili kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo.

RC Macha amesema kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha inashirikiana vyema na wakulima pamoja na Vyama vya Kilimo na Masoko (AMCOS) ili kuwasaidia wakulima waongeze uzalishaji wa zao la pamba kwa angalau wazalishe kuanzia kilo 1200 au zaidi na hivyo kukuza uchumia wao na pato la Mkoa kwa ujumla.

“Niwapongeze kwa juhudi zenu za uzalishaji wa zao hili la pamba, lakini niwahakikishie kwamba Serikali iko pamoja nanyi bega kwa bega kuhakikisha kwamba tunainua na kuongeza kiwango cha uzalishaji ili angalau kila mmoja wetu azalishe kuanzia kilo 1200 za pamba, na kwa kufanya hivyo kutakuza uchumi wa familia zetu pamoja na Mkoa wetu,” amesema RC Macha.

RC Macha akiwa ameambatana na Mhe. Mboni Mhita ambaye ni DC wa Kahama amewaasa wakulima walime pamba kwa kuzingatia utaalamu na watumie viuatilifu ili pamba wanayovuna iwe bora na iendane na kiwango walicholima kwani Serikali inajitahidi pia kutafuta bei nzuri ya pamba wanayozalisha kadiri iwezekanavyo na kuona kwamba zao hili linarudisha heshima na thamani yake kama ilivyokuwa awali.

Pia amewasisitiza Maafisa Ugani wa Halmashauri ya Ushetu kuendelea kushirikiana vizuri na wakulima pamoja na kufanya ufuatiliaji na mwenendo wa uzalishaji wa zao hilo pamoja na kuhakikisha dawa za kuulia wadudu, bomba za kupulizia wadudu pamoja na mbegu za pamba zinapatikana kwa wakati na kugawiwa kwa usawa ili wakulima wazalishe kwa tija.

Kando na hayo, ameendelea kuwakumbusha pale wanapopata faida baada ya kuuza pamba waweze kutunza kiwango fulani cha pesa kwa ajiri ya kilimo cha msimu unaofuata pamoja na kutumia vizuri pesa kuboresha maisha ya familia zao.

Kwa ujumla, kata ya Uyogo ina idadi ya wakulima wa pamba takribani 799, hekari zilizolimwa mpaka sasa ni takribani 2003, pia mbegu zilizopokelewa ni zaidi ya Tani 33.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa