• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Serikali yaamua kuwawekea dhamana wanunuzi wa Pamba

Posted on: July 15th, 2019

Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga amesema Serikali ya Tanzania kupitia Benki kuu, imeamua kuweka dhamana kwa kufidia hasara itakayopatikana kwa wanunuzi wa Pamba kwenye soko la Dunia ili waweze kununua Pamba kwa bei ya shilingi 1,200 kwa kilo.

Akizungumza na Viongozi wa Mkoa na Wakulima kwa nyakati tofauti leo tarehe 15/07/2019 wakati akianza ziara ya siku tatu Mkoani Shinyanga Mhe. Hasunga amesema Serikali imefikia maamuzi hayo katika kikao cha pamoja kati ya Serikali, wanunuzi na baadhi ya wamiliki wa Benki kilichoitishwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Mkoani Tabora jana tarehe 14/07/2019.

"Kuanzia leo, Benki kuu itakuwa inakamilisha taratibu zote na wafanyabiashara wataanza kupewa fedha kwa ajili ya kununua pamba" amesema Mhe. Hasunga.

Aidha, amezidi kueleza kuwa, Serikali imezitaka Benki kupunguza riba kutoka asilimia 16 hadi asilimia 11 ili kuwawezesha wanunuzi kupata fedha za kununua pamba.

Hasunga amesema lengo la Serikali ni kuwasaidia wanunuzi waweze kupata fedha ya kununua pamba yote ya wakulima na wakulima wapate fedha kwa bei ya shilingi 1,200 kwa kilo kama ilivyotangazwa licha ya bei ya soko la Dunia kushuka.

Amewahakikishia wakulima kuwa, vituo vyote kutakuwa na fedha za kutosha kununua pamba na wakulima watapata fedha zao moja kwa moja na pia kuanzia mwaka ujao kutakuwa na mfumo mzuri zaidi wa ununuzi wa pamba usiokuwa na usumbufu kwa wakulima na wanunuzi.

Akielezea changamoto zilizotokana na wanunuzi kushindwa kununua pamba katika msimu huu, Mhe. Hasunga amesema kuwa Serikali ilitangaza bei ya sh. 1,200 kwa kilo baada ya kukokotoa na wanunuzi na kuona bei katika soko la Dunia ipo juu, lakini kutokana na vikwazo mbalimbali bei ya soko la Dunia imeshuka hivyo wakulima watapata hasara iwapo watanunua kwa bei hiyo, pia Benki zilikataa kuwapa fedha kwa kubaini hasara hiyo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amebainisha kuwa, Shinyanga ndiyo Mkoa wenye viwanda vinavyomilikiwa na wazawa ni vema pia kuzungumza na wenye viwanda hivi kufahamu wanahitaji kiasi gani ili waweze kununua pamba inayozalishwa Mkoani hapa. 

Akizungumza na wakulima katika kiwanda cha Afrisian kilichopo Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Telack amewataka wakulima kuhakikisha wanaitunza vizuri pamba ili isishuke ubora wake, kwani pamba ya Tanzania inasifika kwa ubora na nyuzi zinazofaa kwa kutengeneza nguo.

Mhe. Hasunga yupo Mkoani Shinyanga kwa siku tatu ikiwa ni ziara ya kikazi, pamoja na shughuli nyingine atatembelea vituo vya kununulia pamba.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa