• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SIMAMIENI UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO - RC MNDEME

Posted on: October 10th, 2023

Na. Shinyanga RS.

MKUU wa mkoa wa shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme amefanya kikao kazi na Maafisa Tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji kwa lengo la kuwakumbusha majukumu yao ya kazi ikiwemo kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, utatuzi wa kero za wananchi, kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato, kueleza umma juu ya fedha wanazopokea kutoka serikali kuu, utunzaji wa mazingira na kupambana dhidi ya ukatili wa kijinsia katika maeneo yao.

Mhe. Mndeme ameyasema hayo leo tarehe 10 Oktoba, 2023 wakati alipokutana na wataalam hao katika ukumbi wa mikutano uliopo shule ya savannah plains huku akiwasisitiza kwenda kuzingatia maadili na nidhamu huku akikemea tabia ya kuchati na simu wanapokuwa wakiwahudumia wananchi huku akisisitiza kuwa kipaumbele cha serikali ni utoaji wa huduma bora kwa wananchi wenyewe na ndiyo maelekezo ya Mhe. Rais.

"Nendeni mkasimamie utekelezaji wa miradi ya maendeleo, mkatoe elimu juu ya utunzaji wa vyanzo vya maji na mazingira, tatueni kero za wananchi, toeni taarifa za mapokezi ya fedha za serikali pia mkaongeze bidii katika kukusanya wamapato ya serikali katika maeneo yenu," alisema Mhe. Mndeme.

Katika hatua nyingine Mhe. Mndeme amewaeleza wataalam hao kuwa serikali ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeleta zaidi ya Trilioni moja fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali huku akiwataka kwenda kuzisimamia ili zililete matokeo chanya kwa wananchi katika maeneo yao.

Aidha amewataka wakurugenzi wa halmashauri zote za mkoa huu kuhakikisha wanalipa stahiki za watumishi wao, kuandaa mafunzo ya watumishi, kutatua kero za wananchi na watumishi katika halmashauri zao ili wamsaidie Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ndiyo maelekezo yake huku akiwataka kuchapa kazi kwa bidiii zaidi.

Kwa upande wao wakurugenzi wa halmashauri hizi za mkoa wa shinyanga wamekiri kupokea maelekezo ya Mhe. Mndeme na kumuahidi kuwa wanakwenda kuyatekeleza maelekezo yote ikiwemo utatuzi wa migogoro na kulipa stahiki za watumishi wao.


HABARI PICHA



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa