• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SINA MUHALI NA YEYOTE ANAYECHEZA NA ZAO LA PAMBA - RC MACHA

Posted on: November 16th, 2024

Na. Paul Kasembo, KISHAPU

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amesema kuwa hatokuwa na muhali na mtu yeyote atakayejaribu kucheza au kukwamisha kwa namna yoyote juhudi za kurudisha heshima ya kilimo cha zao la pamba katika Mkoa wa Shinyanga, huku akiwapongeza wananchi, viongozi wa Kijiji cha Mwamishoni Kata ya Bubiki, Jeshi la Polisi na Maafisa kilimo kwa ujumla wao kwa kufanikisha ukamatwaji wa gari hili ambalo lina mbegu za pamba.

RC Macha ameyasema haya tarehe 16 Novemba, 2024 alikuwa akikagua mbegu za pamba ambazo kwa mujibu wa Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP) Fraterine Tesha ambaye alimwakilishi RPC Shinyanga SACP Janeth Magomi kwamba mbegu hizi mifuko 107 iliyokuwa imebebwa kwenye gari (FUSO) namba T 618 DRJ ambayo baada ya kukamatwa imehifadhiwa katika Kituo cha Polisi Wilaya ya Kishapu.

"Sintokuwa na muhali na mtu yeyote ambaye kwa namna moja au nyingine atajaribu kukwamisha juhudi za kurejesha heshimu ya zao la pamba hapa mkoani Shinyanga, na katika hili nitaanza na hawa wote walioshiriki kwenye tukio hili la mbegu za pamba katika Chama Cha Ushirika Mwamishoni hapa Kishapu," amesema RC Macha.

Kando na mifuko 107 ya AMCOS ya Mwamishoni, kulibainika uwepo wa mifuko mingine zaidi yenye takribani Kilo 660 za mbegu za pamba ambazo haifahamiki wamiliki wake baada ya RC Macha kuamuru upekuzi zaidi kati gari hili ambapo zilikutwa chini ya hiyo mifuko 107 ikiwa katika mifupo mchanganyiko.

Kufuatia kugundulika kwa mifuko hii zaidi kumemlazimu Macha kumuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude kuunda Timu maalum kufuatilia, kukagua na kutoa taarifa ya kila AMCOS ilitakiwa kupata mifuko mingapi ya mbegu, imepata mingapi na imebakiwa na mingapi kwa mchanganuo sahihi.

Baada ya sakata hili, kumempelekea RC Macha kwenda kukutana na wananchi wa Mwamishoni ambapo kupitia mkutano wa hadhara amewahakikishia kuwa Serikali yao ipo makini sana na kwamba hata uwepo wa mbegu zinazodhaniwa kuwa siyo halisi ilikwishaanza kufanyiwa kazi na sasa matunda yake wameyaona kuwa kumbe mbegu halisia za msimu huu wa 2024/2025 zipo na sasa zitagawiwa kwao bure.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa