• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TUMIENI MAFUNZO HAYA KUONGEZA TIJA KATIKA KAZI ZENU - HILDA.

Posted on: June 3rd, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MRAJIS Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Shinyanga B. Hilda Boniphace amewataka viongozi na washiriki wa Bodi za Vyama vya Ushirika vya Mazao ya Bustani (HORTCULTURAL AMCOS) ambao wameanza mafunzo ya siku mbili katika Ukumbi mdogo wa Mikutano uliopo Lyakale Hotel kuyatumia vizuri mafunzo haya ili yakalete tija zaidi katika utekelezaji wa shughuli zao huku akisisitiza ifike wakati waondokane na soko la ndani peke yake, waweze kuzalisha zaidi na kusafirisha nje ya nchi kwani wanao uwezo huo.

Hilda ameyasema haya leo tarehe 3 Juni, 2024 alipokuwa akifungua mafunzo haya yaliyojumuisha viongozi 18 ambao wamekuwa wakishughulika na kilimo cha mbogamboga na matunda katika Kijiji cha Bugalama, Kata ya Bugalama Halmashauri ya Wilaya ya Msalala na kuhudumia Mgodi wa Bulyanhulu kupitia.......

"Twendeni tukayatumie vizuri mafunzo haya ili yalete tija na kuleta ubunifu wenye kuinua uchumi wa mmoja mmoja na Uahirika kwa ujumla katika kutekeleza shughuli zenu za kilimo cha mbogamboga na matunda, kwani uwezo huo mnao na Serikali imefungua fursa zaidi katika kuuza bidhaa hizi nje ya nchi," amesema Bi. Hilda.

Bi. Hilda amesema kuwa Vyama vya Mazao ya Bustani ni vichache sana, na kwakuwa wao wameonesha uwezo mkubwa katika kuhudumia Mgodi ni wakati wao sasa kwenda kuboresha zaidi mara baada ya mafunzo haya na ndiyo lengo kuu la mafunzo haya wanayopatiwa na ukizingatia kuwa hata Serikali imetilia mkazo mkubwa zaidi kilimo cha matunda na mbogamboga ambapo Wanaushirika au kikundi waweza kunufaika zaidi.

Kwa upande wake Ndg. Justin Mogendi ambaye ni muwezeshaji na mtoa mada kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika - Dodoma amsema kuwa Serikali imejipanga vizuri sana kuhakikisha kuwa biashara ya zao la mbogamboga na matunda linaimarika zaidi ndani na nje ya nchi na ndiyo sababu hata wao pamoja na wadau wengine wamekutana hapa.

Katika Mafunzo haya mada mbalimbali zitafundishwa na Justin Mogendi - TCDC, Spania Nyobuya - TCDC, Justine Mallo - COASCO SHINYANGA, Laurent Mikama - TAMISEMI na Mafy Tickin - MoCU SHINYANGA.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa