• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

VETA SHINYANGA, ANZISHENI KITENGO MAALUM CHA KUIMARISHA UWEZO WA KUJITEGEMEA - RC MACHA

Posted on: November 22nd, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ameushauri uongozi wa Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Shinyanga (VETA) ukiongozwa na Mwl. Abraham Mbughuni kuanzisha na kusajili Kitengo Maalum cha Kuimarisha Uwezo wa Kujitegemea (Self Reliance Unity) kitakachokuwa na wajibu wa kubuni na kutekeleza kazi mbalimbali kwa kutumia rasilimali walizonazo ikiwemo wanachuo, mitambo na wakufunzi lengo likiwa ni kuzalisha kipato cha chuo huku akisema kuwa Serikali itafanya kazi pamoja nao ikiwa ni pamoja na kuwapatia zabuni za kujenga miradi ya Serikali.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 22 Novemba, 2024 wakati wa Mahafali ya 43 hafla iliyofanyika katika Viwanja vya VETA Shinyanga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Dini, wazazi/walezi, watumishi wa VETA, wananchi na wanachuo wenyewe ambapo pamoja na mambo mengine amewataka wahitimu kwenda kuchangamkia fursa za mikopo ya Serikali isiyokuwa na riba pamoja na kuchapa kazi kwa bidii zaidi.

"Pamoja na pongezi kwako Mkuu wa Chuo na watumishi wote, lakini niwatake sasa kuanzisha Kitengo Maalum cha Kuimarisha Uwezo wa Kujitegemea (Self Reliance Unity) ambacho kitasajiliwa na kutambulika chenye lengo la kuzalisha, kukiwezesha chuo hiki kufanya kazi za nje, kuongeza pato na kukifanya chuo kujitegemea na kuchechemua uchumi wenu kupitia Fani mnazofundisha ikiwemo utengenezaji wa barabara na Serikali itafanya kazi pamoja nanyi na kuwashika mkono kwa kuwa mna kila kitu hapa ikiwemo mitambo mizito ya kutekelezea kandarasi za aina yoyote," amesema RC Macha.

Akitoa taarifa ya Chuo, Mwl Abraham amesema kuwa VETA Shinyanga ina jumla ya Ekari 19 zenye Hati Miliki, mazingira rafiki, tulivu na yenye kuvutia kwa kufundishia, kujifunzia, kupumzikia, mabweni, vyumba vya madarasa, karakana, maeneo ya kufundishia pamoja na kutoa taaluma kwa fani ya uendeshaji mitambo mizito, magari, uchomeleaji na uunganishaji vyuma huku akiwakaribisha wananchi kuleta kazi zote zinazohusu fani hizo kwani VETA inapokea na kutekeleza kwa ufanisi na weledi mkubwa zaidi.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa