• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

VIJANA NA WASOMI MKOANI SHINYANGA, IGENI MFANO WA BBT KISHAPU - RC MACHA

Posted on: February 18th, 2025

Na. Paul Kasembo, NGOFILA - KISHAPU

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka vijana wasomi mkoani hapa kuiga mfano wa vijana wa Jenga Kesho yako Bora (BBT) waliopo Kata ya Ngofila wilayani Kishapu ambao waliamua kujitolea na kuitumia elimu na maarifa yao yote katika kusaidia wakulima na kuamua kulima mashamba yao ya mfano kwa wakulima ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa taaluma waliyoipata Chuoni na kwenye mafunzo maalum ya BBT.

Hayo ameyasema leo Februari 18, 2025 wakati wa ziara ya kukagua na kuhamasisha kilimo cha zao la pamba katika Kata ya Ngofila wilayani Kishapu ambapo ametembelea Kijiji cha Mwamanota, Idushi na Ngofila ambapo huko amekutana na vijana hao wenye ari, nguvu na moyo wa dhati wa kutumia elimu na muda wao wote katika mashamba ya wakulima na ya kwao ikiwa ni sehemu ya kujipatia kipato, kujiajiri na hivyo kuwa sehemu ya mfano na chachu kwa vijana wengine.

"Niwashauri vijana na wasomi wetu mkoani Shinyanga, njooni muige na kujifunza namna bora ya kujiajiri na kutumia vema nguvu, elimu na maarifa mliyonayo huku Kata ya Ngofila wilayani Kishapu ambapo kuna vijana wenzenu kutoka kundi la Jenga Kesho iliyo Bora ambao wameamua kujitolea na kutumia elimu, maarifa na muda wao kuwasaidia wakulima katika kilimo cha pamba na wao pia kulima mashamba ya mfano ikiwa sehemu ya kujiajiri na kuongeza pato binafsi," amesema RC Macha.

Aidha, RC Macha amesema kuwa kwa sasa atakuwa anapatikana zaidi vijijini ambako ndiyo walipo wakulima na kwamba atatumia muda mwingi zaidi kuhamasisha na kuwatia moyo wakulima wote ili kuhakikisha heshima na hadhi ya pamba mkoani Shinyanga inarejea kama ilivyokuwa hapo awali, kwani pamba (dhahabu nyeupe) ni sehemu ya utambulisho wa Mkoa wa Shinyanga.

Akitolea mfano wa shamba la Raphael Zengi  mkulima wa Kijiji cha Ngofila ambaye msimu wa 2023/2024 alipata kilo 4605 kwa hekari 4 ambapo ni wastani wa kilo 1150 kwa hekari moja, RC Macha amesema huo ndiyo mlengo na nia ya Serikali ya kuhakikisha kila mkulima anapata kuanzia kilo 1000 au zaidi kwa hekari moja.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa