• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Waganga Wakuu Waagizwa kila Hospitali kuwa na Dawa za Wazee

Posted on: July 26th, 2017

Waganga Wakuu wa Mikoa yote wameagizwa kuhakikisha kila Hopitali inakuwa na dawa maalumu kwa ajili ya wazee pamoja na kuwabaini Wazee wote ili wapate huduma za afya bila malipo.

Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Hamis Kigwangala ametoa agizo hilo alipotembelea kituo cha Wazee kilichopo katika Manispaa ya Shinyanga Mkoani hapa hivi karibuni. 

" Hakuna maana yoyote kama mzee anapimwa na tatizo lake linafahamika halafu akifika kwenye dirisha la dawa anaambiwa dawa zimeisha kanunue" amesema Kigwangala.

Mhe. Kigwangala amewahakikishia Wazee kuwa, Serikali itahakikisha hali ya upatikanaji wa huduma za jamii, chakula, malazi na dawa inaimarika ikiwemo mikakati madhubuti ya kuwapatia huduma bila malipo na kuwalinda. 

Amesema kulingana na sensa ya mwaka 2013 idadi ya Wazee nchini ni milioni 2.5 ambayo ni sawa na asilimia 5.6 ya wananchi wote na inakadiriwa kuongezeka na kufikia wazee 2.7 mwezi Desemba, 2017, hivyo Wizara inasimamia maslahi na kuhakikisha wanapata haki zao za msingi.

Awali, Mwenyekiti wa kituo cha Wazee Kolandoto Mzee Somola Maganga na Katibu wa Wazee Mkoa wa Shinyanga Mzee Sengerema wameishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa jitihada kubwa ya kuwajali wazee na kutekeleza yale waliyoomba. 

Aidha, Wazee hao wameomba kuwa na Daktari bingwa wa magonjwa ya wazee hususani ugonjwa wa tezi dume ambapo Waziri amewahakikishia kuwa, hospitali lazima ziwe na dawa maalumu kwa ajili ya wazee pamoja na kuwepo madaktari.

Kuhusu watumishi wa Idara ya ustawi wa jamii, Mhe. Kigwangala amesema Wizara itaendelea kushughulikia changamoto zinazowakabili ili waweze kutekeleza majukumu yao vema.

Katika ziara hiyo, Naibu Waziri ameweka jiwe la msingi ujenzi wa bweni la wazee wa kituo cha Kolandoto litakalobeba wazee 20, amefungua jiko la gesi, amekabidhi bajaji pamoja na kiboksi cha huduma ya kwanza kwa wazee hao.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa