• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

Posted on: February 12th, 2025

Paul Kasembo, SHY RS.

KAMISHNA wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Shinyanga Ndugu Leo Komba amewaomba wananchi na wadau wote wa kodi Mkoani Shinyanga kulipa kodi ya pango la ardhi kwa wakati ili kuepuka riba ya 5% itokanayo na adhabu na badala yake wakilipa italeta maendeleo ya Taifa na ufanisi wa kazi za Wizara kwa ujumla huku akisisitiza kuwa mwananchi akilipa kwa wakati hakutakuwq na malimikizo jambo ambalo linapelekea mwananchi kuona kama kodi ni kubwa.

Ameyasema haya leo Februari 12, 2025 kwenye Kikao na Wadau wa Kodi Mkoa wa Shinyanga kilicholenga kupokea, kujadili chanagmoto wanazokabiliana nazo, kuzifahamu na hatimae kuweka makubaliano ili hatimae kulipwa kwa madeni hayo ambayo yanatajwa kuwa ni muda mrefu sasa .

“Wananchi, niwaombe sasa muwe na utamaduni wa kuhakikisha kwamba mnalipa kodi ya pango la ardhi kila mwaka na kwa wakati ili kuepuka riba itokanayo na kuchelewa jambo ambalo kwa sehemu kubwa mnalalamika kuwa ni kubwa, lakini kumbe mngelipia kwa wakati hayo yote yasingekuwepo, na kwa kufanya hivyo kunawezesha Taifa kuimarisha na kuboresha zaidi utoaji wa huduma kwa wananchi," amesema Leo Komba.

Aidha amewataka wadau kuwa na kawaida ya kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Ardhi pale wanaposhindwa kuendeleza matumizi ya ardhi wanayomiliki ili Mamlaka husika iwapatie wadau wengine waiendeleze na kulipa kodi kwa maendeleo ya Taifa.

Kwa upande wake Afisa Ardhi Mwandamizi Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi. Halima Nassor amewasihi wananchi kuweka kipaumbele na utamaduni wa kulipa kodi kwa wakati kwani Serikali imeanza utekelezaji wa kutoa Hati Madai za siku 14 kwa watu wote wenye malimbikizo ya kodi ili wajadiliane na kukubaliana kulipa kabla ya kuanza kuchukua hatua za kisheria.

Kwa mujibu wa Kamishna wa Ardhi Msaidizi ndugu Leo Komba, Mkoa wa Shinyanga unadai wadau wake zaidi ya Tzs. Bilioni 3.5 huku akitoa wito kwa wananchi ambao bado wanadaiwa kutumia muda huu wa siku 14 ambazo zimetajwa kuwa ni kipindi cha njia shirikishi ambapo mdeni atapata nafasi ya kwenda ofisi za ardhi na kulipa au kukubaliana namna ya kulipa.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa