• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI TUNZENI AMANI YA NCHI YETU - RC MACHA

Posted on: July 25th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ametoa wito kwa wananchi wote kujitahidi kuitunza amani na utulivu wa nchi yetu ili kuendelea kuwaenzi Mashujaa wetu kwani ikipotea huwa ni vigumu sana kuirejesha, na hata ikirejea haiwezi kuwa kama ilivyokuwa awali huku akiwasisitiza kutenda yaliyomazuri zaidi ili tutakapoondoka tuendelee kukumbukwa kama Mashujaa ambao leo ni maadhimisho yao.

RC Macha ametoa wito huu leo tarehe 25 Julai, 2024 wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa Tanzania  ambapo kwa Mkoa wa Shinyanga yamefanyika katika Viwanja vya Mashujaa (Mazingira Center) na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, vyombo vya Usalama, viongozi wa dini, wananchi na watu,ishi wa Serikali.

"Nitoe wito wangu kwenu wananchi wote, tujitahidi sana kuendelea kuitunza amani yetu na kuenzi utulivu wa nchi yetu ili isipotee na kutoweka kwa namna yoyote ile, kwani ikiwa hivyo ni vigumu sana kuirejesha na hata ikirejea haiwezi kuwa kama ilivyokuwa awali," amesema RC Macha.

Aidha RC Macha amesema kuwa, waweza kuwa na mali nyingi sana lakini unapokosa amani na utulivu ni sawa na mateso wakati wote kwani huwezi kufurahia chochote kile huku akiwataka wananchi kutosubiria mtu aondoke ndiyo wampongeze, badala yake wampongeze akiwa hai kwani kuna mifano mingi ya mashujaa wa sasa hivi na mfano mzuri ni Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ametenda mengi mema kwa ajili ya wanashinyanga na watanzania kwa ujumla wakena hivyo tunapaswa kumpongeza, kumtia moyo na kumuombea sana ili aendelee kuwatumia vema wananchi wote.

Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa Tanzania huadhimishwa kila ifikapo tarehe 25 Julai, 2024 ikiwa ni sehemu ya kuwaenzi wale wote waliopoteza maisha yao kwa ajili ya kulipigania na kuhakikisha kunakuwa na amani na utulivu ndani ya Taifa letu. 


@shinyangamanispaa @kahamamc_official @shinyangadc_official @kishapudc @msalaladc2023 @ushetudc @shinyanga_tanzania

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa