• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wananchi wa Kahama wamshukuru Rais Magufuli kwa kuwachangia ujenzi wa shule

Posted on: January 8th, 2020

Wananchi wa Kahama wamshukuru Rais Magufuli kwa kuwachangia ujenzi wa shule

Shule ya msingi Mayila iliyopo Mtaa wa Mayila, kata ya Nyihogo Wilaya ya Kahama imefunguliwa rasmi huku wananchi wa kata hiyo wakimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli kwa kuwachangia shilingi mil. 5 ili kuhakikisha shule hiyo inakamilika.

Wazazi hao wametoa shukrani hizo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack alipokwenda kukagua utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais la kuhakikisha shule hiyo inafunguliwa mapema jana tarehe 07 Januari, 2020.

Wamesema kuwa, kukamilika kwa shule hiyo kutawapunguzia adha ya umbali wa zaidi ya kilomita 3 watoto wa kata hiyo waliokuwa wanalazimika kuvuka barabara kubwa kufuata shule kata za jirani hali iliyopelekea kuwa katika hatari ya kugongwa na magari.

“Nashukuru sana kwa shule hii, watoto wetu mwanzo walikuwa wanakwenda mbali na sisi kama wazazi tupo tayari kuendelea kushirikiana na Serikali kujenga maboma” amesema Bw. Richard Joseph.

Diwani wa kata ya Nyihogo Mhe. Shadrack Mguami amesema, “kuna wakati naamka usiku kumuombea Mhe. Rais, sikutegemea kupata fedha kutoka kwake kwani angeweza kufanya shughuli nyingine lakini akaona atoe hapa, tunaahidi tutaendelea kumuunga mkono kwa kujenga maboma” 

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kahama Mji Bw. Anderson Msumba amesema watoto zaidi ya 200 wameandikishwa kuanza darasa la kwanza hivyo uhitaji ni mkubwa, hata hivyo Halmashauri inaendelea kukamilisha maboma 108 na kufunga shule mpya 8.

“Tunamshukuru Mhe. Rais ametupa mori kuhakikisha shule hii inafunguliwa” amesema Msumba.

Mhe. Rais alichangia shilingi milioni 5 ili kuongeza nguvu ya kukamilisha shule hiyo alipopita Wilayani Kahama akielekea Wilayani Chato mwezi Novemba, mwaka jana 2019 na kuagiza ifunguliwe mwezi Januari mwaka huu 2020.

Shule hiyo iliyokuwa na vyumba viwili vya madarasa, hivi sasa ina vyumba 8 na matundu ya vyoo 12.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa