Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WASICHANA 198,865 KUNUFAIKA NA CHANJO - SHINYANGA

Posted on: April 19th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

Muwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude amesema kuwa jumla ya ya wasichana 198,865 wamelengwa kufikiwa na kupatiwa Chanjo ikiwa ni lengo la asilimia 80 katika kipindi cha tarehe 22 hadi 28 Aprili, 2024 ambayo ni wiki ya chanjo Afrika huku akitoa wito kwa wazazi na walezi kujitokeza kupeleka watoto wao ili wawezekupatiwa chanjo hii muhimu.

Mhe. Mkude amesema kuwa Kampeni hii ina lengo la kuongeza kinga kwa wasichana wenye umri kati ya miaka 9 hadi 14 ambqpo watapatiwa chanjo dozi moja (1) ambapo awali walikuwa wakipatiwa dozi mbili (2) na sababu ya mabadiliko haya ni matokeo ya tafiti za kisayansi zilizothibitisha kuwa dozi moja ya HPV inatosha kutoa kinga kamili dhidi ya maambukizi ya saratani ya mlango wa kizazi.

"Mkoa unatarajia kutoa chanjo kwa wasichana 198,865 Kampeni ambayo tutaianza rasmi tarehe 22 hadi 28 Aprili, 2024 itakayolenga wasichana wenye umri wa miaka 9 hadi 14 na itafanyika katika Shule za Msingi na Sekondari za Serikali na zisizo za Serikali," amesema Mhe. Mkude.

Utekelezaji wa chanjo hii unatajwa kuwa ni mkakati muafaka katika kutokomeza kabisa maradhi na kupunguza vifo vya watoto, na hivyo kupunguza gharama kubwa ambazo familia za Kitanzania zingetumia katika kutibu maradhi yatokanayo na magonjwa yanayozuilika kwa chanjo huku akiwaagiza Watendaji ngazi zote wahakikishe wasichana wote walio nje ya shule wanapatiwa chanjo hii.

Nchini Tanzania chanjo hii iliidhinishwa mwaka 2014 na kuanza kutumika rasmi mwaka 2014 katika Mkoa wa Kilimanjaro ambapo baadae mwaka 2018 ilianza kutumika nchi nzima kwa kutoa dozi mbili (2). Chanjo hii imeidhinishwa na Shirika la Afya Duniani na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kwa matumizi ya binadamu.


HABARI PICHA


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa