• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akamilisha ziara yake Mkoani Shinyanga

Posted on: July 17th, 2018

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amekamilisha ziara yake ya siku tano Mkoani Shinyanga leo tarehe 17 Julai, 2018. 

Mhe. Majaliwa katika ziara yake, iliyoanza tarehe 13 Julai, 2018 ametembelea Halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga na kuzungumza na Watumishi wa Umma ambapo amewakumbusha wajibu wao katika kuwatumikia wananchi kwa kuwa waadilifu na waaminifu.

Katika Halmashauri zote Mhe. Majaliwa pia ameweza kukutana na wananchi ambapo amewaeleza mipango na kazi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano katika kuwaletea maendeleo pamoja na kuwaahidi kuzidi kuboresha utendaji, miundombinu ya maji, afya, elimu, umeme na barabara.

Baadhi ya shughuli alizozifanya ni pamoja na kuzindua mradi wa maji katika kijiji cha Isoso Wilaya ya Kishapu, kutembelea na kuona viwanda vya kuchambua pamba, kutengeneza mafuta katika Manispaa ya Shinyanga na kiwanda cha kuchambua mchele Halmashauri ya Mji Kahama, kuona ujenzi wa vituo vya Afya na kuzindua soko na ghala la wakulima katika kata ya Chela.

Aidha, Mhe. Majaliwa amezindua mpango wa kutoa Bima ya Afya kwa Wakulima kupitia vyama vya Ushirika ambapo Kitaifa uzinduzi umefanyika katika kijiji cha Kangeme, kata ya Ulowa, Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu.

Mhe. Majaliwa ambaye aliambatana na Naibu Waziri wa Ujenzi Mhe. Elias Kuandikwa pamoja na Naibu Waziri wa OR- TAMISEMI Mhe. Joseph Kakunda na viongozi wengine ametoa maagizo mbalimbali kwa viongozi na watendaji Mkoani hapa ikiwemo kuwafuata wananchi mahali walipo na kutatua kero zao badala ya kukaa Ofisini.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa