• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAZIRI WA MADINI MHE. DOTTO BITEKO AFUNGUA ZAHANATI YA NYAMISHIGA NA KUKABIDHI KWA WANA NYAMISHIGA GARI LA KUBEBEA WAGONJWA VIKIWA NA THAMANI ZAIDI YA TZS. MILIONI 280.

Posted on: July 3rd, 2023

Na. Shinyanga RS.


Waziri wa Madini Mhe. Dotto Mashaka Biteko amefungua Zahanati iliyojengwa na Kikundi cha Wanawake Wachimbaji Wadogo wa Madini (TAWOMA MSHIKAMANO GROUP) na kukabidhi Gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) kwa wananchi wa Kata ya Lunguya litakalotumika katika Zahanati ya Nyamishiga vyenye thamani ya zaidi ya Tzs. Milioni 280 kwa Halmashauri ya Msalala Mkoani Shinyanga huku akiwaahidi kuwapatia Leseni ya uchimbaji Madini.

Mhe. Biteko ameyasema hayo leo tarehe 3 Julai, 2023 katika hafla hiyo iliyofanyika katika Kijiji cha Nyamishiga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwamo Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme, Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita, viongozi wa Dini, Chama cha Mapinduzi, wachimbaji na wananchi ambapo pamoja na kuwapongeza sana wana kikundi wa Mshikamano lakini pia aliwaeleza namna ambavyo Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anavyowajali wachimbaji wadogo wakiwamo wa Lunguya.

"Mimi niseme tu kuwa, Serikali ya Chama cha Mapinduzi kupitia Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiye aliyeruhusu ninyi mchimbe na sasa niseme tu kuwa katika hili nasema kwa ujari na furaha kubwa kuwa ninyi mnastahili kupewa Leseni, mnastahili kuchimba ili mshiriki uchumi wa madini Mhe. Rais anawapenda sana wana Shinyanga na hata sasa amewaletea viongozi wachapa kazi kweli kweli Mhe. Christina Mndeme anayajuwa madini na haki za wachimbaji anazijuwa pamoja na Mkuu wa Wilaya Mhe. Mboni Mhita ni mpambanaji sana ," alisema Mhe. Biteko.

Aidha TAWOMA MSHIKAMANO walimpongeza sana Mhe. Mndeme kwa namna anavyowajali wachimbaji hao huku wakiomba kujwngewa uzio, kupelekewa umeme na maji ilimkuboresha huduma za kijamii.

Kwa upande wake Mhe. Mndeme alisema kuwa Serikali ya Mkoa wa Shinyanga inawajali sana wachimbaji wadogo wadogo na kwamba suala la ukosefu wa huduma ya maji na umeme amelipokea huku akitumia jukwaa hilo kuwaahidi kupeleka huduma hizo kama walivyoomba.

"Nawaagiza RUWASA NA TANESCO Mkoa wa Shinyanga kuleta huduma ya maji na umeme katika Zahati hii na Eneo hili ili wananchi hawa waendelee kupata huduma hizi muhimu, na kuhusu uzio tutajenga kwa mwaka wa fedha ujao kupitia Halmashauri yetu ya Msalala hivyo wananchi ondoeni hofu kabisa Serikali ipo nanyi," alisema Mhe. Mndeme

Kukamilika kwa Zahanati hii kunakwenda kuwaondolea usumbufu na adha waliuokuwa wakiipata wananchi hawa ambapo walilazimika kutembea umbali wa Kilomita 10 kwenda kufuata huduma ya matibabu katika Kituo cha Afya Lunguya.

Awali wananchi walianza ujenzi wa Zahanati hii mwaka 2018 ikiwa ni sehemu ya kupambana na kukabiliana na usumbufu huo unaotajwa kudumu kwa muda mrefu kwa kutumia nguvu kazi zao wenyewe ambapi jumla ya zaidi ya 21 zilichangishwa kupitia Sungusungu ambazo zilitumika kujenga jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje yaani OPD

Ilipofika Machi, 2022 kikundi cha Mshikamano kilianza rasmi ukamilishaji wa Zahanati hii ambayo inatajwa kwenda kuwahudumia wananchi zaidi ya 4970.

















Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa