• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

FUTAZIKA AFUNGUA MAFUNZO YA AWALI YA UALIMU NA UAMUZI WA MPIRA WA MIKONO

Posted on: August 2nd, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

AFISA Elimu Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi ndg. Dedan Rutazika aliyemuwakilisha Dafroza Ndalichako ambaye nji Katibu Tawala Msaidizi, Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mkoa wa Shinyanga amefungua rasmi mafunzo ya awali ya ualimu na uamuzi wa mpira wa mikono kwa walimu kutoka shule mbalimbali za msingi na sekondari mkoani Shinyanga huku akiwasisitiza kwenda kuyatumia vema mafunzo watakayoyapata hapa ili yawe na tija katika shule wanazotoka.

Rutazika ameyasema haya leo tarehe 1 Agosti, 2024 katika shule ya sekondari Uhuru ambapo mafunzo haya yanafanyika na kuhudhuriwa pia na baadhi ya walimu kutoka Mkoa wa Simiyu na shule binafsi ikiwemo Kom Sekondari mafunzo ambayo yanaongozwa na Mkufunzi wa mchezo huu kutoka Chama cha Mpira wa Mkojo Taifa (TAHA) ndg. Emmanuel Majura.

"Niwasisitize sana walimu wetu ambao mnapata taaluma hii hapa na kupitia mafunzo haya muende kuyatendea haki kwa kuhakikisha yanaleta tija zaidi katika maeneo mnayotoka ili lengo la mafunzo haya likaonekane kwa vitendo na kwa kufanya vizuri katika mashindano yajayo mwaka 2025 kwakuwa ninaimani elimu hii itakuwa imewafikia kwa sehemu kubwa sana wanafunzi wetu hivyo watafanya vizuri zaidi," amesema Rutazika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Mkono Mkoa wa Shinyanga ndg. Mtaki Musiba amesema kuwa maoni, ushauri na maelekezo wamepokea na watakwenda kuyafanyia kazi ili lengo la kuinua na kukuza wanamichezo wa mpira wa mkono Mkoa wa Shinyanga linafanikiwa.

Aidha Bi. Jesca Simuchile ambaye ni Afisa michezo Mkoa wa Shinyanga amesema kuwa uwepo wa mafunzo haya ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo aliyeelekeza kuanzishwa kwa program maalum ya kuibua, kukuza na kuimarisha michezo mashuleni ikiwemo na mchezo wa mpira wa mkono mkoani Shinyanga kwani michezo ni afya, ajira na huleta amani.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa