• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Maktaba ya Video

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 14th, 2025

    Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, ametoa wito kwa wafanyabiashara na wawekezaji kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo katika Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kukuza uchumi wa mkoa huo na Taifa kwa ujumla.Mhe.

     Mhita ametoa wito huo leo Novemba 13, 2025 wakati wa Mkutano ulioambatana na uzinduzi wa Baraza la Biashara la Mkoa wa Shinyanga, uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wawakilishi wa sekta binafsi, wafanyabiashara na wadau wa maendeleo.

    Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mhita ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Mkoa wa Shinyanga, amesema Mkoa huo umejaliwa kuwa na rasilimali nyingi na fursa za uwekezaji katika sekta mbalimbali zikiwemo kilimo, mifugo, madini, viwanda na biashara, hivyo kuna haja ya kuzitumia fursa hizo kikamilifu kwa maendeleo ya uchumi wa mkoa na Taifa.

    “Napenda kuwahamasisha wawekezaji kutoka ndani na nje ya mkoa kuchangamkia fursa zilizopo, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya pamba, bidhaa za mifugo, pamoja na huduma za kijamii kama shule, hospitali na hoteli. Pia, Mkoa umetenga maeneo rasmi ya uwekezaji likiwemo eneo la Buzwagi Special Economic Zone ambalo tayari limepata leseni kutoka TISEZA,” amesema Mhe.

     Mhita.Aidha, Mhe. Mhita amesisitiza kuwa Mabaraza ya Biashara ni majukwaa muhimu yanayowakutanisha wadau wa sekta binafsi na Serikali kwa pamoja kujadili namna bora ya kuboresha mazingira ya biashara na kutatua changamoto zinazokabili sekta hiyo ili kuimarisha mchango wake katika kukuza uchumi.

    Awali, akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Kamishna wa Polisi Salum Hamduni, alieleza kuwa mabaraza hayo ni daraja muhimu kati ya Serikali na Sekta Binafsi katika kubaini changamoto na fursa mbalimbali kwa maendeleo endelevu ya kiuchumi.

    Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) Mkoa wa Shinyanga, Bw. Jonathan Manyama, aliipongeza Serikali kwa jitihada zake katika kuboresha mazingira ya biashara.

  • SHINYANGA IKO SALAMA, WANANCHI JITOKEZENI KUPIGA KURA KWA AMANI - RC MHITA

    October 20th, 2025

    Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, amewatoa hofu wananchi wa mkoa huo kuhusu hali ya usalama kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025, akisisitiza kuwa mkoa uko salama na hauna tishio lolote la kiusalama.

    Akizungumza katika kikao na waandishi wa habari kilichofanyika kwenye ukumbi wa Virgimack Hotel, Mhita amesema Serikali ya Mkoa imejipanga kikamilifu kuhakikisha zoezi la kupiga kura linafanyika kwa amani, utulivu na haki bila bughudha kwa mpiga kura yeyote.

    “Natoa rai kwa wananchi wa Shinyanga kujitokeza kwa wingi kutumia haki yao ya kikatiba. Serikali tupo tayari, vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vipo macho kuhakikisha siku hiyo inapita kwa amani. Hakuna tishio lolote la kiusalama,” amesema Mhita.

    Amesisitiza kuwa yeyote atakayebainika kuchochea vurugu au vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani atachukuliwa hatua kali za kisheria mara moja, ili kulinda utulivu wa mkoa na kuhakikisha kila mwananchi anatekeleza wajibu wake bila hofu.

    “Tunaendelea kufuatilia kwa karibu mienendo yote ya kisiasa na kijamii. Hatutamvumilia mtu yeyote atakayevuruga amani. Tunataka uchaguzi uwe wa heshima, utulivu na unaoendana na maadili ya taifa letu,”

    aliongeza.Aidha, alisisitiza kuwa amani ni msingi wa maendeleo, na kwamba hakuna mkoa au taifa linaloweza kupiga hatua kiuchumi au kijamii pasipo utulivu.Kwa upande wake, aliwataka waandishi wa habari kushirikiana na Serikali katika kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kushiriki uchaguzi kwa amani, pamoja na kutoa taarifa sahihi na zinazojenga umoja wa kitaifa.

  • SHUHUDIA ULIPOFIKA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE SHINYANGA, RC MHITA ATEMBELEA UJENZI WAKE, NDEGE KUBWA.

    October 16th, 2025

    Hatimaye ndoto ya wananchi wa Shinyanga kushuhudia huduma za usafiri wa anga ikitolewa kwa ukamilifu inakaribia kutimia!

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • Next →

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa