• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Profesa Mbarawa awaahidi maji ya uhakika wananchi wa Mwakitolyo na Kishapu

Posted on: July 5th, 2019

Waziri wa maji Mhe. Profesa Makame Mbarawa amewahakikisha wananchi wa vijiji vya Mwakitolyo, Wilaya ya Shinyanga na Kishapu Wilayani Kishapu kuwa tatizo la kukosa maji litakuwa historia baada ya kupewa ahadi hiyo kwa muda mrefu bila ya mafanikio.

Akizungumza na wananchi wa vijiji hivyo kwa nyakati tofauti wakati wa ziara yake Mkoani hapa jana tarehe 04/07/2019, amewaeleza wananchi wa kijiji cha Kishapu kuwa, Serikali inatambua shida ya maji ya muda mrefu inayowakabili hivyo Mamlaka ya Maji Kahama na Shinyanga (KASHWASA) itaanza kujenga mradi katika Wilaya ya Kishapu kwani ina uwezo mkubwa wa kujenga miradi ya maji bila kutumia wakandarasi ambao wanatumia muda mrefu.

"Serikali pesa tunayo na nitaitoa pesa hiyo hivi karibuni, hivi sasa hatutaki msubiri tena kwa muda mrefu, tuliahidi na lazima tutekeleze Ilani" amesama Prof. Mbarawa. Amesema haiwezekani wananchi wa Kishapu wapate shida wakati bomba lipo kilometa chache kutoka hapo.

Aidha, akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mwakitolyo Mhe. Mbarawa amesema anajipa miezi mitatu pamoja na KASHWASA kuhakikisha mradi wa maji kutoka kwenye bomba kubwa la maji ya ziwa Viktoria uliopo kilometa 13 kutoka kijijini hapo unakamilika. "Nimetembea maeneo mengi lakini hapa kweli mna shida ya maji, ndoo moja sh. 500 hii haikubaliki, mradi wa awali haukuwa na uwezo kwa sababu mkandarasi na mshauri walifanya ujanja na wizi wa kupindukia"

Amesema yeye akiwa mwenye dhamana ya kuhakikisha wananchi wanapata maji hivyo Serikali imeamua kubadilisha miundombinu yote ya mradi wa awali ambao umeshindwa kufanya kazi na kuanza upya ujenzi wake na kuweka bomba jipya na pesa tayari ipo.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa