• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

Posted on: May 23rd, 2025

#shinyanga_rs

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amesema kuwa uwepo wa Mafunzo ya Mpango wa Elimu Changamani kwa Vijana Walio nje ya Shule - IPOSA ni mkombozi kwa vijana walio wengi ambao wanaokosa fursa ya elimu ya kawaida, kwani inawezesha kupata stadi za maisha, ujasiliamali, na ufundi wa awali hivyo kuwaandaa kwa ajili ya kujiajiri na kuajiriwa.

Akizungumza Mei 23, 2025 wakati wa halfa ya ufungaji wa mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku 21 na yaliyolenga kuwajengea uwezo walimu na viongozi wa elimu mkoani Shinyanga, Mhe. Macha alilipongeza sana Shirika la Kimataifa la Korea International Agency (KOICA) kupitia Serikali ya Korea Kusini kwa kuwajengea uwezo viongozi hao ili wakatekeleze kwa ufanisi Programu hiyo muhimu.

"Kwa dhati kabisa tuseme, uwepo wa Mafunzo ya Mpango wa Elimu Changamani kwa Vijana Walio nje ya Shule - IPOSA ni mkombozi kwa vijana walio wengi ambao wanaokosa fursa ya elimu ya kawaida  kwani inawezesha kupata stadi za maisha, ujasiliamali, na ufundi wa awali hivyo kuwaandaa kwa ajili ya kujiajiri na kuajiriwa wao wenyewe," alisema Mhe. Macha.

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) kwa ufadhili wa KOICA kupitia Serikali ya Korea Kusini kunatajwa kuwaongezea maarifa zaidi vijana ambapo watafundishwa kusoma,  kuandika, kuhesabu, mafunzo ya ufundi stadi pamoja na ujasiliamali.  Lengo ni kuwasaidia kuondokana na changamoto za ukosefu wa ajira na kuwawezsha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii zao.

Awali Mkurugenzi wa Taasisi ya TEWW Profesa Philipo Sanga alisema kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau wake itaendelea kuboresha Sekta ya Elimu huku akisisitiza kuwa mafanikio ya awamu ya kwanza ya IPOSA yaliwavutia wadau wengi na hivyo KOICA imeamua kuendelea kufadhili awamu ya pili ya program hii na ambayo itawafikia vijana walio wengi zaidi katika Mikoa mbalinbali ikiwemo Shinyanga.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

    May 20, 2025
  • SERIKALI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU SITA NA MAJERUHI 11 KATIKA AJALI YA MGODI WA MWAKITOLYO.

    May 18, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI, NENDENI MKAWE MABALOZI SAHIHI WA KAZI ZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – RC. MACHA

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa