• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC Shinyanga awaonya Bodaboda wanaolaghai watoto wa kike

Posted on: January 31st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amewaonya waendesha pikipiki, maarufu kama Bodaboda wenye tabia ya kuwapakia wanafunzi hasa wa kike na kuwalaghai matokeo yake kuwapa mimba za utotoni.

Mhe. Telack ametoa onyo hilo mapema leo tarehe 31 Januari, 2019, wakati akitoa hotuba ya kufunga mradi wa “DREAMS – Innovation Challenge, keeping girls in Secondary schools” uliokuwa unatekelezwa na shirika la “amref health Africa” kwa miaka miwili katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, Wilaya ya Kahama.

“Suala la bodaboda tumeshalisema sana, itabidi kukaa vikao na viongozi wa bodaboda, vijiwe vya boda boda vilivyopo karibu na shule viondolewe, watafute wateja siyo wanafunzi” amesema Telack.

Akisisitiza jambo hilo Mhe. Telack amewataka Wakuu wa Wilaya kuhakikisha bodaboda wenye tabia ya kuwapatia “lift” wanafunzi wa kike waache mara moja na wakibainika wakamatwe.

Aidha, amewahimiza wanafunzi watembee kwenda shule badala ya mazoea ya kupanda bodaboda ili kuwaepusha na vishawishi visivyo vya lazima.

Amesema, mtoto wa kike ni rasilimali, hivyo wakiachwa bila uangalizi ni kuharibu Taifa la baadaye matokeo yake hata familia zao hazitadumu kutokana na kuanza ngono mapema.

Katika hotuba yake, Mkuu wa Mkoa pia ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kuendeleza mazuri yaliyofanywa na mradi wa DREAMS ili kuwasaidia wanafunzi hasa wa kike, kwani uelewa wa afya ya uzazi umewasaidia sana kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya UKIMWI kwa vijana kutoka asilimia 2.5 mwaka 2016 hadi 0.8 mwaka 2018.

Mradi wa DREAMS uliowafikia wanafunzi katika shule 15 ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Msalala, umepunguza tatizo la watoto wa kike walioacha shule kwa sababu ya mimba kutoka wanafunzi 79 mwaka 2016 hadi wanafunzi 38 mwaka 2018.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa