• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

AFISA UTAMADUNI MKOA AKUTANA NA MAAFISA UTAMADUNI WA HALMASHAURI ZA MKOA WA SHINYANGA KUJADILI UBORESHAJI WA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA MAKTABA ZA VIDEO

Posted on: October 21st, 2025

Na Johnson James Shinyanga

Maafisa Utamaduni kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Shinyanga wamekutana leo katika ukumbi mdogo wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwenye kikao kazi maalum kilichofanyika kwa lengo la kujadili namna bora ya kusimamia maktaba za video, pamoja na kubadilishana uzoefu kuhusu ukusanyaji wa mapato kupitia maktaba hizo, pamoja na vyanzo vingine vya mapato.

Kikao hicho kimefanyika chini ya uratibu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Kitengo cha Utamaduni, ambapo ajenda kuu zilijikita katika kutoa elimu ya utafiti kwa wamiliki wa maktaba za video na kujadili changamoto na mafanikio katika ukusanyaji wa mapato kwenye halmashauri mbalimbali.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Afisa Utamaduni wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Janeth Elias Mompome amesema sekta ya Sanaa kupitia maktaba za video ni miongoni mwa maeneo yenye mchango mkubwa kwenye mapato ya halmashauri, lakini bado yanakabiliwa na changamoto za usimamizi, ufuatiliaji na usajili rasmi wa wamiliki.

"Ni muhimu sasa kuimarisha usimamizi wa maktaba hizi kwa kushirikiana na wamiliki wake. Kupitia utafiti na elimu kwao, tutaweza kuongeza mapato halali ya serikali na kukuza sekta ya utamaduni kwa ujumla," alisema.

Washiriki wa kikao hicho walipata nafasi ya kuwasilisha uzoefu wa kila halmashauri juu ya namna wanavyokusanya mapato kutoka kwa wamiliki wa maktaba hizo, changamoto wanazokutana nazo, pamoja na mapendekezo ya maboresho ya mifumo ya usimamizi.

Miongoni mwa mapendekezo yaliyotolewa ni pamoja na kuanzisha utaratibu wa kutambua rasmi maktaba zote zinazofanya kazi katika mkoa, kuwaelimisha wamiliki kuhusu umuhimu wa kulipa ushuru halali, na kutumia mfumo wa kidigitali katika kufuatilia shughuli zao kwa uwazi zaidi.

Kikao hicho pia kimeweka msingi wa kuandaa mkakati wa pamoja wa mkoa wa kusimamia sekta ya video libraries kwa ufanisi zaidi, huku msisitizo ukiwekwa kwenye ushirikiano baina ya halmashauri, wamiliki na mamlaka nyingine zinazohusika na masuala ya sanaa na utamaduni.

MWISHO

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa